juu

Monday, 3 June 2019

MATUMIZI HOLELA YA DAWA YANAVYOSABABISHA SARATANI

KITENDO cha mwanamke kutumia kiholela dawa za uzazi wa mpango humuweka katika hatari kiafya hasa kupata kansa ya kizazi.  Kibaiolojia wanawake wana uwezekano mkubwa kupata saratani kwa kiwango cha asilimia 100 kuliko wanaume. Tatizo hilo linahusishwa zaidi na homoni ya Oestrojeni ambayo kiasili wanawake ndio ambao wanazo zaidi kuliko wanaume.

Dawa za uzazi wa mpango zinatakiwa kutumiwa vizuri kwa ushauri wa daktari kwani kuna wengine zinawasumbua. Kuna mabinti na wanawake wanakwenda tu kujinunulia wenyewe kwenye maduka ya dawa, hiyo ni hatari kwao. Dawa zozote ni lazima upatiwe na daktari kwa sababu yeye anao uwezo wa kukuangalia na kukutathmini.

Mara nyingi dalili za kansa huanza kujitokeza mtu anapokuwa na umri kati ya miaka 15 hadi 20 lakini kwa kuwa wengi hawana mwamko wa kupima afya zao mara kwa mara hugundulika kuwa na ugonjwa hasa wakiwa na umri wa kuanzia miaka 40. Kwa asilimia tano tu mtu huweza kupata ugonjwa huo kwa kurithi kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Kitendo cha mama anayetakiwa anyonyeshe kutonyonyesha mtoto kunaongeza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani ya matiti. Matiti kwa mwanamke yana kazi kuu mbili, kwanza ni kutengeneza chakula kwa ajili ya mtoto wake lakini pili ni kutengeneza umbo lake (urembo).

Tatizo tunaloliona leo hii la saratani ni kwa sababu wanawake wengi hawapendi kunyonyesha watoto wao kwa hofu ya kupoteza ule mwonekano wao, bila kujua kwamba kufanya hivyo kunasababisha kuharibu mpangilio wa mwili na hivyo kuwa kwenye hatari ya kupata saratani.

Kuna visababishi vingine ambavyo kwa kiwango kikubwa vinachangiwa na mfumo mbovu wa maisha yetu ya kila siku. Vyakula vya kusindikwa vyenye kemikali vilivyo kwenye makopo au chupa na mafuta mengi vinavyosababisha ongezeko kubwa la uzito wa mwili na vinywaji vyenye sukari nyingi inaweza kuwa sababu ya kupata saratani. Sababu nyingine ni uvutaji wa sigara na matumizi ya bidhaa zilizotengenezwa kwa kutumia tumbaku, unywaji wa pombe na matumizi ya maji yaliyochafuliwa kwa kemikali (water pollution) ni chanzo cha saratani.

Vitu hivyo huharibu mpangilio wa seli na kuuvuruga. Kibaiolojia mwili wa binadamu umejengwa kwa chembechembe hai ziitwazo seli ambazo ndizo hutengeneza viungo mbalimbali na mfumo mzima wa mwili wa binadamu. Chembechembe hizo huwa na tabia ya kugawanyika, kukua na kupevuka ili ziweze kutengeneza mwili na kwamba huwa kuna mpangilio maalumu wa jinsi zinavyokua, kugawanyika na kupevuka kulingana na wakati.

Sasa inapotokea utaratibu huo wa kawaida ukavurugika basi hapo seli hizo hukua, hugawanyika na kupevuka bila mpangilio maalumu na hivyo kusababisha saratani. Saratani ni ugonjwa ambao upo katika kundi linalojumuisha magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza ambao husababisha vifo vya idadi kubwa ya watu. Kwa upande wa hii saratani ya matiti takwimu za dunia zinaonesha inashika nafasi ya pili duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa.

Kasi ya ugonjwa inaonekana kuwa juu zaidi na inakadiriwa ifikapo mwaka 2030 ikiwa hatua hazitachukuliwa kukabiliana na ugonjwa huo, idadi itaongezeka mara dufu kufikia asilimia 50 katika nchi zinazoendelea.

Saratani hiyo inashika nafasi ya pili kwa kundi la wanawake kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa na inashika nafasi ya nne kati ya saratani zote zinazogundulika nchini. Hali hiyo inachangiwa na uelewa mdogo wa jamii juu ya ugonjwa huo pamoja na imani potofu kwa wengi kukimbilia kwa waganga wa kienyeji wakidai wamerogwa.

Hata wale wanaofika hospitalini huwa wapo katika hatua mbaya hivyo matibabu yake huwa ni magumu. Wale wanaowahi katika hatua ya kwanza na ya pili ya ugonjwa wakipatiwa matibabu hupona kabisa lakini si hatua ya tatu na nne.

DALILI ZA UGONJWA

Kwa kuwa yale ni mabadiliko ya chembechembe hai mara nyingi huwa yanatokea ndani ya mwili ambako hatuwezi kuona dalili kwa nje katika hatua ambayo zimeanza kukua au kugawanyika, tunachoweza kuona kwa nje ni uvimbe, ongezeko la titi, uzito wa titi na maumivu makali.

Uvimbe unapokuwa mkubwa wakati mwingine husababisha kukandamizwa kwa mishipa ya damu na inapopasuka chuchu huanza kutoa damu.

Uvimbe huweza pia kubadili mwonekano wa chuchu na kuzifanya ziwe kama ganda la limao wakati mwingine huvuta chuchu kwa ndani na au kuzifanya kuwa ngumu. Pia zinaweza kutoa kidonda na uvimbe ukiwa mkubwa zaidi husambaa kuelekea sehemu za kwapani, ukichelewa kupata matibabu saratani husambaa hadi kwenye viungo vingine vya mwili ikiwamo mifupa, mapafu na hata moyo.

MATIBABU

Ili kuuondoa uvimbe mgonjwa hufanyiwa upasuaji. Matibabu ya pili huwa ni kuwapatia tiba ya mionzi ili kuzuia seli ambazo hazikuonekana awali.

Saratani huwa inasambaa kwa njia ya damu na kwa kuwa zina tabia hii, huwa wagonjwa wanapatiwa dawa ya saratani za dripu (Chemotherapy), wale wenye vichocheo vingi vya homoni huwa tunapewa Hormonaltherapy pia dawa za kutuliza maumivu na nyinginezo kulingana na hali ya mgonjwa husika.

USHAURI

Ni muhimu kuzingatia ulaji unaofaa hasa vyakula vyenye virutubishi vinavyohitajika mwilini, mazoezi mara kwa mara, kunywa maji ya kutosha na kupima afya mara kwa mara.

 Na mtaalam wetu, A.Mandai

The post MATUMIZI HOLELA YA DAWA YANAVYOSABABISHA SARATANI appeared first on Global Publishers.


Share:

UKIMPATA MTU SAHIHI, MSHIKILIE KWELI KWELI

Moja kati ya kosa kubwa ambalo watu wengi wanalifanya ni kutothamini hisia. mahusiano mengi yamevunjika kwa sababu tu ya mmoja kati ya wapendanao kutotambua umuhimu wa penzi lao na mwisho wa siku wanajikuta wameachana. Mimi na wewe msomaji wangu ni mashahidi wa hili. Kwenye dunia ya wapendanao sasa hivi, wengi sana wamejikuta kwenye majuto baada ya kushindwa kushikamana kwenye mikono salama.

Mwanamke anaweza kuwa kwenye uhusiano na mtu sahihi, anakikuta amemuachia. Vivyo hivyo mwanaume, anaweza kuwa na mtu sahihi katika uhusiano wake lakini anajikuta ameipoteza bahati ya kuwa na mpenzi wake huyo hadi mwisho wa safari sababu tu ya kushindwa kuheshimu umuhimu wa safari yao. Hii inatokana na mtu kuleta mazoea kwenye penzi. Wakati mwingine inasababishwa na dharau ya mtu. Anapomuona mwenzake anamheshimu, anampenda na anamthamini, kwake inageuka kama fimbo ya kumchapia.

Analeta maringo, anaanza kuleta pozi na inapotokea mwenzake amekata tamaa na kuanzisha uhusiano mwingine, anajikuta akijilaumu. Kwamba alikuwa na mtu sahihi lakini hakumthamini na matokeo yake anataka kurudisha majeshi lakini anakuwa ameshachelewa. Ndugu zangu, thamani ya mtu mara nyingi huwa inaonekana pale anapokuwa hayupo.  Anapokuwepo unaweza kuwa unamchukulia poa lakini akiondoka unaanza kumkumbuka na kutambua ule uwepo wake na kuona kwamba haukupaswa kuupoteza. Kwa nini usubiri majuto? Kwa nini usiitumie vizuri leo yako ili uweze kuishi vizuri na mtu ambaye ndio chaguo lako.

Mtu ambaye kweli unampenda kutoka moyoni. Mtu ambaye moyo wako ukiwa naye unapata furaha, unaachaje kumjali? Kwa nini usimtunze kama mboni ya jicho lako? Kabla ya kumfanyia vituko, kabla ya kuanza kumuonesha kejeli, dharau na mambo mengine kama hayo, hakikisha unajiuliza mara mbilimbili kwamba ninayemfanyia hayo yote anastahili? Jiulize je,  uliye naye ni mtu sahihi kwako? Unampenda kwa dhati? Na yeye anakupenda kama unavyompenda wewe? Anakujali? Hana kipingamizi chochote cha kuwa na wewe? Mnaelewana? Ukipata majibu chanya kuhusu maswali hayo, shikamana na huyo mtu. Ninasema shikamana naye sababu naye anastahili

kushikamana na wewe. Mpende, mthamini na umuone ni mtu wa muhimu katika dunia hii kuliko kitu chochote. Mueleze naye aujue umuhimu huo maana jahazi lenu litakapoangamia, mtaishia kujilaumu. Mnayo nafasi kabla ya kulaumiana, msiruhusu kisingizio cha shetani. Mkataeni huyo shetani sababu Mungu amewapa akili na upeo wa kutambua mema na mabaya. Heshimu hisia za mwenzako ili naye akuheshimu. Kila iitwayo leo, fanya jambo kwa ajili ya kuonesha upendo kwa mwenzako.

Aone unamjali na unamthamini. Hata kama si jambo kubwa, fanya hata dogo. Mathalani unaweza hata kumjulia hali baada ya kupita ukimya wa muda fulani. Mpigie simu muulize anaendeleaje, ameshindaje na mambo mengine madogomadogo ambayo yanaweza kumfanya mwenzako ahisi unamjali. Guswa na matatizo yake.

Kama anaumwa, mjulie hali ya kuumwa kwake ikiwezekana hata baada ya saa fulani kupita. Mpe zawadi ndogondogo au hata kubwa kulingana na uwezo wako. Mfanye mwenzi wako kila siku akufurahie maana furaha yake ni wewe. Akiikosa kwako ataipata wapi kwingine? Mpende kwelikweli kama hutapenda tena.  Usimtegee, mrudishie upendo kama anavyokupenda wewe. Tambua uwepo wake hata unapokuwa mbali naye. Heshimu dhamira na mipango yenu mliyojiwekea. Usikubali hata kidogo kumpoteza mtu ambaye mna mipango ya kufika mbali katika uhusiano wenu.

Kwa leo naishia hapa. Tukutane wiki ijayo. unaweza kunifuata kwenye mitandao yangu ya kijamii, instagram na facebook natumia jina la erick

The post UKIMPATA MTU SAHIHI, MSHIKILIE KWELI KWELI appeared first on Global Publishers.


Share:

Sunday, 2 June 2019

Angalia kile kitabia cha kufuta namba kwenye simu kilivyomponza huyu jamaa

Related image

Angalia kile kitabia cha kufuta namba kwenye simu kilivyomponza huyu jamaa

Jana nilijipa kazi ya kufuta vitu visivyo na umuhimu kwenye sm yangu. Katika futa futa si nimefuta namba ya bosi wangu. Halafu boss mwenyew wa kike. Mida ya Saa mbili usiku nikawa chumbani kwangu. Mara simu ýÀñgΓΉ ikawa inaita. Kucheki namba ngeni. Nikapokea baada ya salamu. Me→nani mwenzangu?? Boss→we hunijui me ?? Me→usinijbu swali kwa swali Nita kublacklist sasa hiv. Sipendagi ujinga.. Kwa sasa nazurura tu mtaani na roba langu La machupa

πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚


Share:

Sifa 10 za mwanaume ambaye kila binti anayetaka aolewe angependa aolewe naye!!

Related image

Sifa 10 za mwanaume ambaye kila binti anayetaka aolewe angependa aolewe naye!!

SIFA 10 ZA MWANAUME AMBAYE KILA BINTI ANAETAKA KUOLEWA ANGEPENDA AOLEWE NAE.
1. Awe na pesa nyingi
2.Siyo lazima awe mzuri wa sura
3. Ajenge ukweni
4.Awe mpole
5.Asimuonee wivu mke wake
6.Awe mwenye upendo wa dhati
7.Asishike simu ya mke wake.
8.Akimkuta na mwanaume apite tu, akitaka kujua ni nani asubiri nyumbani
9.Awe anamskiliza mke wake kwa kika kitu.
10.Asipende mwanamke mwingine zaid yake
UKIMPATA MWANAUME MWENYE SIFA HIZO KAPIME DNA LAZIMA ATAKUWA NI BABA AKO.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚


Share:

Saturday, 1 June 2019

SMS nzuri sana ya Kimahaba

Related image

Nimekuapata! Kama unanichukia, nipige mshale, lakini
tafadhali si moyoni sababu hapo ndipo wewe ulipo.
Share:

Siwema wa Nay wa Mitego Akanusha Kumtelekeza Mwanaye

Image result for Siwema wa Nay wa Mitego

MZAZI mwezie na mwanamuziki mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay’, Siwema Edson amekanusha madai ya kutomtembelea mwanaye Cartes.


Akizungumza na gazeti hili, Siwema alisema huwa ana ratiba maalum ya kwenda kumuona mwanaye huyo ambaye anaishi na bibi yake, ambaye ni mama yake na Nay, ila anapokwenda huwa hamjulishi mzazi mwenzake huyo.


“Mtoto wangu naongea naye kila mara na nimeshaenda kumuona zaidi ya mara tatu, sema tu baba yake hajui hivyo angekuwa anamuuliza mama yake angempa jibu, lakini mwanangu nishamuona na ninaongea nae kila mara,” alisema Siwema.

Stori: Imelda Mtema
Share:

KUMUOTA EX WANGU MARA KWA MARA INATOKANA NINI?

Related image

Habari za Majukumu!?

Nilikuwa na Mpenzi wangu wa Tangu Shule ya Msingi tupo wote, Sekondari Pia, Tukahitimu Tukarudi uraiani Tukiwa wote, Baadae yeye Alibahatika kupata kazi kabla yangu Akaondoka Mkoani, Baada ya miaka miwili Nami nilipata kazi Baada ya mafunzo kumalizika Nikapangiwa Mkoa Fulani, Cha Ajabu nilipofika Mkoa huo Nikakutana na baadhi ya vijana tulikuwa wote huko Nyumbani wakaniambia Kuwa Huyo binti Yupo Mkoani Hapa nilipopangwa kikazi Kwa vile Baada yeye kupata kazi Tulipoteza mawasiliano , Sasa nikaona Haina Haja Kumtafuta, Ila Siku Moja ktk Majuku ya kazi tulikutana Live kila mmoja anamshangaa mwenzie Kutokana na majukumu yetu Hayaruhusu kusogeleana Kwa Muda ule baada ya majukumu kuisha, Ililazimu tuonane tupeane Mawasiliano upya Mahusiano Yalianza Upya tena ila Mwenzangu niligundua kuwa Yupo tofauti sana ni mtu wa Sitarehe sana na ni maisha ambayo Sikuyapenda kabisa na tayari aliishapata Mchumba Huku Huku na huyo mchumba wake nae inaonekana ni mtu wa Sitarehe sana kamwambukiza huyo Binti Kukesha kwenye kumbi za Starehe kwake kawaida tu! Sasa, alitaka Amuache yule jamaa yake ili Tuanze maisha wawili kutoka na ile Tabia ya Starehe sana kibaya zaidi Tayari Keisha kuwa mnywaji wa Pombe Na Mimi situmii kilevi chochote Nikaona, Nikaona Japo Nampenda Kweli lakini nikiingia kwenye ile ndoa nitajutia hadi kufa nikamwambia Afunge ndoa Na yule jamaa yake Mimi nitatafuta mwingine, Kweli baadae Walioana lakini Alikuwa ni msumbufu sana kwangu hata baada ya kuolewa na mpaka Leo imepita miaka 3 toka Aolewe tatizo ni kuwa Namuota sana kwa wiki lazma iwe Mara 2 au 3 Tena naota ndoto za furaha sana mpaka Huwa nacheka ndotoni kutoka na Ndoto zile za maisha ya furaha nae, Asbh Wife wangu Huniambia Usiku ulikuwa unaota Unacheka nashindwa cha kumjibu zaidi kuishia kucheka tena Sasa Swali langu ni hili 

HII INATOKANA NA NINI? NA NI MUDA SANA HATUKO PAMOJA NA ISIJE KUWA USIKU HUWA NAONGEA MANENO YA MAHABA NDOTONI WIFE ANAYASIKIA ITAKUWA INAMUUMIZA SANA.

Share:

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger