juu

Saturday 31 August 2019

Hizi ndio sehemu 10 zenye msisimko mkali zaidi kwenye mwili wa mwanamke








Share:

USHAURI: NIMESHIKA SIMU YA MPENZI WANGU, SINA HAMU


Mimi ni kijana umri miaka 26 mchumba wangu anafanya kazi katika kampuni moja hivi ya binafsi ,japo hatujaoana lakin tuna kawaida ya kutembeleana mara kwa mara,yeye anaishi Kinondoni Mkwajuni mimi naishi Ubungo Riverside,

Weekend hii nilienda kumtembelea akanipa simu yake nimwekee vocha nikiwa naweka vocha nikashangaa sms inaingia "honey uko wapi". Sikumwambia chochote na wala sikuifingua iyo sms ila niliweza kuisoma coz simu yake ni smartphone aina ya Sony yaan sms ikitumwa uwa inapita kwa juu unaweza kuisoma yote.

Niliamua kufungua whatsApp yake nikaanza kupitia baadhi ya chatting zake cha ajabu nikakutana na chatting moja amechat na mwanaume nilijua ni mwanaume coz niliangalia profile picture yake na sms zao zilinitsha sana jamaa kuna sms anasema " Juzi nilifurah mno nilipokuingizia nyuma" halafu mchumba wangu alisms akajibu". Mwenzio sijazoea nyuma". Kuna sms nyingine jamaa alituma akisema " Mwezi wa 6 inabd nikutie mimba".Daah niliishiwa pozi lakini sikusema kitu chochote hadi leo bado niko kimya nafikiria cha Kufanya......

Naombeni ushauri wenu






Share:

JIHADHARI NA MAADUI WA PENZI LAKO

NIjumaa nyingine murua. Siyo mbaya kwa wanajamvi hili, ndugu, jamaa na marafiki kushirikiana katika mapenzi kama vile wakati wa sherehe au msiba.

Pia siyo mbaya kujuliana hali na kutambulishana mambo ya msingi yanayoendelea kwenye uhusiano wako na mpenzi wako.

Hata hivyo, kuna wakati watu wengine wa pembeni, wawe majirani, ndugu, wazazi au marafiki wanaweza kuwa sumu ya uhusiano wako, hasa pale unapowategemea sana kutoa msaada, maoni au maelekezo katika maisha yako ya kimapenzi. Kuna mambo ya msingi unayoweza kufanya ili kupunguza uwezekano wa rafiki, ndugu, jamaa au wazazi kuwa kuvuruga penzi lako.

Kwanza kabisa ni kujitahidi kudhibiti taarifa zenu kwenda kwa wengine; kadiri unavyoelezea uhusiano wako kwa watu wengine ndivyo unavyowapa nafasi watu kutoa maoni na hata kudhani kuwa wana dhamana ya kukuelekeza unavyotakiwa kuishi na mwenza wako.

Katika eneo hili, chukua muda wa kutosha kutafakari na kufanya uchunguzi kuhusu masuala yako ya uhusiano kabla hujaanza kutafuta maoni na ushauri kwa wengine. Ni bora ukasoma vitabu, na mada mbalimbali, hususani zihusuzo tabia na maisha ya uhusiano, zitafakari vema ili kuona zinahusiana vipi na unayokumbana nayo katika mahusianao yako.

Pili ni lazima uwe na uwezo wa kufanya mambo yako kipekee; Tambua kuwa tabia ya mpenzi wako inaweza kuwa ni ya kipekee, mazingira pia ya tukio linalokufanya utake ushauri au maoni kwa wengine yanaweza kuwa ni ya kipekee, hivyo ushauri au maoni utakayopokea yanaweza yasikusaidie moja kwa moja katika suluhisho lako. Ukitambua hili, utafanya bidii ya kujenga uwezo binafsi wa kuchambua tatizo unalokumbana nalo katika uhusiano na kutafuta suluhisho kabla ya kutegemea watu wengine.

Tatu ni lazima ujue mwenye uamuzi ni wewe; ni kweli kwamba kuna nyakati ni muhimu kupata ushauri kutoka kwa watu wengine na zaidi sana watu wenye uelewa sahihi na unaowaamini, hakikisha kuwa unatambua kuwa wewe mwenyewe ndiye mwenye kubeba lawama ya uamuzi utakaochukua.

Nne ni lazima uwe na subira; Usichukue uamuzi wa haraka katika uhusiano hususan uamuzi wa kuamua kuwashirikisha watu wengine habari ya mambo yahusuyo uhusiano wako. Unapofanya uamuzi wa kuwashirikisha wengine kwa haraka, unajinyima nafasi ya kulichunguza jambo kwa ufasaha, hususan madhara yanayoweza kutokea kwa kuwaeleza wengine au kama ni tatizo, basi kufikiria njia sahihi ambazo ungeweza kuzitumia kupata suluhu ya tatizo.

Tano ni kufungua njia za mawasiliano kati yenu; Pengine chanzo cha wewe kutaka kuzungumza mambo ya ndani yanayohusu uhusiano wenu kwa watu wengine ni kwa kuwa umekosa nafasi ya kuzungumza kwa ufasaha na mwenzi wako. Tafuteni nafasi za kutosha, jengeni mazingira ya kuzungumzia mambo yenu kabla ya kutaka kuwashirikisha wengine.

Sita ni vyema kuwa peke yenu; Hata kama hutaki kueleza watu kuhusu mambo yanayoendana na maisha yenu, mazingira unayoishi yanaweza kuchangia watu kutaka kuingilia uhusiano wenu kwa kutoa maelekezo, ushauri au maoni kuhusu muishivyo wewe na mpenzi wako. Inapobidi hakikisha hamuishi karibu na wazazi wenu, ndugu au rafiki wa karibu.

Au hufanyi kazi na mwenzi wako sehemu moja, kwani hiyo itakuwa njia rahisi sana ya watu kuona mnavyoishi. Inapobidi kuwa karibu na watu wengine, hakikisha mnakubaliana wewe na mwenza wako namna bora ya kuendesha mawasiliano kati yenu mbele za watu, ili msiwape nafasi ya wao kuanza kutoa maelekezo ya vile wanavyoona mnapaswa kuishi.






Share:

MAMBO YA KUFANYA MPENZI WAKO AKIKUFANYIA KISIRANI

KWA watu waliopo katika uhusiano wa kudumu, watakubaliana na mimi kwamba kuna wakati huwa inatokea mwenzi wako anaamua tu kukufanyia kisirani, na hii inawahusu zaidi wanawake, hataki kuzungumza chochote na wewe. Kila unachomuuliza anakujibu kwa mkato kisha anaendelea na mambo yake, hataki kushirikiana chochote na wewe na hata haki yako ya msingi huipati!

Wengine huweza kudumu kwenye hali hii kwa muda mrefu na kama usipokuwa makini, hii inaweza kuwa sababu itakayowaingiza kwenye matatizo makubwa zaidi. Bahati mbaya ni kwamba ni wanaume wachache sana wanaoelewa nini cha kufanya inapotokea mwanamke unayeishi naye, au unayempenda sana anakubadilikia kiasi hiki.

Yaani unamuona kabisa hayupo sawa, hakuchangamkii, hataki kuzungumza na wewe lakini unapomuuliza kama ana tatizo lolote, anakujibu kwamba hakuna tatizo lolote na yupo sawa. Wengine hudhani kwamba mwanamke husika ameanza dharau, amepata wanaume wanaompa jeuri au hampendi tena!

Kama nilivyosema, ukishindwa kujua hali yake imesababishwa na nini na unatakiwa kufanya nini ili kumrudisha kwenye hali yake ya kawaida, unaweza kujikuta ukisababisha matatizo makubwa zaidi. Kwa hiyo, jambo la msingi unatakiwa kuwa
mwepesi kumsoma mwenzi wako na hii itakusaidia kumgundua muda ambao hayupo sawa.

Ukishagundua kama hayupo sawa na anakuwekea mgomo baridi, muulize kwa upole kama yupo sawa au kama kuna kitu kinamsumbua. Bila shaka majibu yake yatakuwa ni yaleyale, ‘nipo sawa’, ‘hakuna tatizo’ na mengine ya aina hiyo. Ukishamuuliza mara moja au mbili akakujibu vilevile, huna haja ya kuendelea kumuuliza mara nyingi zaidi kwani utasababisha azidi kukasirika.

Kwa jinsi tulivyoumbwa, wanawake wanaongozwa zaidi na hisia. Unapomuudhi mwanamke wako jambo fulani, kitu pekee anachoweza kukifanya kukuonesha kwamba amekasirika, ni kukulalamikia lakini akiona huelewi au kama humpi nafasi ya kulalamika, basi huishia kukununia. Kwa hiyo unapoona amefika katika hali kama hiyo, tambua kwamba kuna ujumbe anataka kukufikishia!

Anataka kukuonesha kwamba umemkasirisha, umemuumiza moyo wake na hafurahishwi na matendo yako. Unachotakiwa kufanya kwanza ni kutulia lakini pili ni kuanza kujichunguza mwenyewe, ni jambo gani umefanya mpaka ukamuudhi? Jiulize mwenyewe ndani ya kichwa chako lakini wakati huohuo, tambua kwamba anahitaji sana ‘attention’ yako.

Mwanamke akinuna, anataka umuoneshe kwamba umeshaelewa kwamba hayupo sawa na unajitahidi kumfanya arudi kuwa sawa! Wengine wanakosea kwamba akishaona amenuniwa, basi na yeye anaanza visa, anaanza kufokafoka na kuwa mkali, hayo ni makosa.

Unatakiwa kushuka chini hata kama bado hujajua kosa lako ni lipi, kuwa mpole kwake, muoneshe kumjali, jitahidi kujiweka karibu naye na mfanyie mambo mazuri. Kama unajiweza, unaweza hata kumuomba mtoke ‘out’, kama amekasirika sana anaweza hata kukataa kutoka na wewe lakini ni jukumu lako kumbembeleza.

Kihulka wanawake wameumbwa kubembelezwa kwa hiyo katika mazingira kama hayo ni nafasi yako ya kuonesha uwezo wako wa kumbembeleza mpaka akubaliane na kile unachokitaka. Ukishapata nafasi ya kutoka naye, au hata kama hamjatoka mpo wenyewe mahali tulivu, anza kuzungumza naye kwa upole ukitanguliza maneno matamu ya kujishusha na kumuomba akusamehe, bila shaka kama kuna jambo umemuudhi atakueleza kwa uwazi, hata kama unaona siyo jambo la msingi sana, rudia kumuomba radhi na mhakikishie kwamba halitajirudia.

Utashangaa anaanza kurudi kwenye hali yake ya kawaida na lile tabasamu lililopotea kwenye uso wake litaanza kuchanua upya. Ukitumia nguvu na ubabe, utakuwa sawa na mtu anayemwagia petroli kwenye moto. Kwa leo ni hayo tu, tukutane wiki ijayo kwa mada nyingine nzuri.






Share:

Mmeachana, Umeachwa ila moyoni bado unahisi unampenda, fanya haya umrudishe na kutengeneza nafasi ya kuwa naye tena.


Hivi karibuni msichana wako ameamua kuachana na wewe au labada wewe ndie uliyeamua kumuacha naye ila baada ya maamuzi hayo kupita na kufanyika, moyoni unahisi upendo wako juu yake bado umeutawala moyo wako na bado anaumiliki tena kwa sehemu kubwa sana na hauko tayari kumwachia aende kwa kuwa umeshaona wazi ya kuwa maamuzi uliyoyafanya au yaliofanyika yana makosa makubwa.

Waulize wanaume imekuandalia njia itakayokusaidia kurudisha muda nyuma na kuwa naye tena, kukurudishia yule mmoja umpendae ambaye juu yake ndio moyo wako unapokamilika, njia hii itategemeana sana na hali ya mwenza wako mlieachana na jinsi anavyojisikia juu yako kwa kile ulichotenda au kumtendea.

#; Yatambue makosa.

Unaweza fikiria unachofikiria kichwani mwako ila lazima huyo msichana atataka kujua ni nini kilichosababisha wewe kubadilika, wanawake wa karne ya digitali huitaji majibu ya sababu sababishi ya kile kilichokusababisha ubadilike kiasi cha huo uwamuzi kufanyika, uwe umesababisha wewe au yeye majibu yanatakiwa, na mwelezee kwa umakini utafanya nini ili kuibadilisha hio hali na kumpa mikakati thabidi na kumuonyesha nia ya kuyatatua hayo matatizo.


#; Omba msamaha na onyesha hisia ya kuwa unamaanisha.

Wanaume wengine hujiona ngangali na kuona hali ya kuomba msamaha ni kujishusha, na inawezekana kabisa alishawahi kukutana hio hali kwenye uhusiano uliopita, muonyeshe una nia ya kubadilika badala ya kujielezea na kuomba msamaha, muonyeshe nia yako kwa matendo, kama ulikuwa unachelewa kupokea simu zake badilika wewe ndo uwe wa kwanza kumtafuta.


#; Mpe muda.

Mpe muda wa kufanya maamuzi yake, maamuzi makubwa kama hayo huwa yanachukua muda kuamuliwa, usiwe na haraka ya kutegemea majibu hapo hapo, kama kweli unamuhitaji mpe muda wa kufanya maamuzi yake mwenyewe iwapo anataka kuwa na wewe au la, inaweza kumchukua sikua au hata wiki mpaka aweze kukuamini tena na kukukabidhi moyo wake, kuwa mvumilivu na usikurupuke na kulazimisha mambo kwani itakuweka mahali pabaya zaidi ya ulipokuwa.




Share:

Hatimaye Sugu Afunga Ndoa Leo








Share:

Mahusiano ya kimapenzi ya umbali na jinsi ya kuyafanya yawe ya mafanikio na furaha.


Usipomuona mpenzi wako kwa muda moyo huingia upweke, matamanio ya kumtaka kumuona huongezeka mara dufu, mawazo ya jinsi alivyo na kila kitu kuhusu yeye hukufanya utabasamu na kufurahia uwepo wake kila umuonapo, na hukupa hisia na tamaa ya kutaka kumuona zaidi na kukufanya hitajio la kuwa naye kukuwa na hamasa zako juu yake kuongezeka na kumpenda zaidi.

Vivyo hivyo iwapo muda mrefu ukipita bila kumuona mpenzi wako upweke huzidi na moyo huchoka, hamasa na taamaa zinabadilika kuwa mzigo, mawazo mazuri ya kimapenzi na husuda hubadilika kuwa msongo, njisi muda unavyozidi kwenda na ndivyo hamasa ya mpenzi wako ndivyo inavyoisha na kuzidi kushuka, moyo unasahau mguso wake aliokuwa nao kwako, shauku ya kuongea inapungua, kama mlikua mnaongea kila baada ya masaa mawili kwenye simu, masaa yatabadilika na kuwa matatu, yakiwa matatu yatabadilika kuwa siku nzima, umbali unakuwa tena hautengenezi upweke wa kutaka kuonana bali unawafanya mioyo yenu kusahauliana na umbali wa hisia kati yenu kuongezeka.
  • Namba 1, Hakikisha unaongea kile kilicho moyoni mwako.
 Wanawake wanauwezo mkubwa wa kugundua iwapo kuna kitu kinakusumbua na vile vile wanawake ni rahisi sana kujihisi, kama wamekugundua umeudhika na usipokielezea mapema akiwa amekuuliza, moja kwa moja ataanza kujifikilia ni yeye ndio aliyesababisha au ni kwa ajiri ya uhusiano kwa sababu yuko mbali unakuwia vigumu ila unakuwa hautaki kuelezea wazi, kwahio kwa mahusiano ya mbali inakubidi uwe mwangalifu na mvumilivu, kama kuna kitu kati yenu hakiendi vizuri, ni vizuri mkakiongea kwa wakati ulio mwafaka, iwapo mkakiacha kikawajengea kinyongo ndani ya mapenzi yenu na kufikia hatua ya kuudhiana, ugonvi wa mapenzi kwa wapenzi walio mbali ni mgumu sana kusuruhishwa.

  •  Namba 2, Hakikisha mnapanga jinsi ya kukutana.
Umuhimu wa kukutana na kuonana ana kwa ana ni mkubwa sana hasa kwa mapenzi ya mbali, kukutana huamsha hisia na mvuto ndani ya mapenzi uliosahaulika, muda ni dawa ya kusahau kwahio iwapo mkiacha kukutana kwa muda mrefu, yale maumivu yanaosababishwa na upweke wa kutomuona mpenzi wako huisha na hamasa za mapenzi pia hupungua, binadamu ameumbwa kubadilika kutokana na mazingira, kwahio mkiruhusu muda mrefu kupita bila kuonana utofauti lazima utaingia kati yenu hata kama mlikua na mapendo makubwa kiasi gani, umuhimu wa kuongea hautokuwepo tena na hisia zitapolomoka na kusababisha mvuto kuisha kabisa ndani ya uhusiano wenu.
  • Namba 3, Fanyeni vitu kwa pamoja mkiwa mbali.
Kwa tekenolojia ilivyongezeka kipindi hichi, hamuhitaji muwe mji au mtaa mmoja ili muweze kufanya kitu cha kuwafurahisha pamoja, tafuteni kitu kipya cha kuongelea iwe filamu au kitu chochote kingine ambacho wote wawili mnafurahia na kupenda kukifanya au kufuatilia, mnaweza pigiana simu na kutaalisha filamu na wote mkaanza kuiangalia kwa wakati mmoja, pande zote mbili mnatakiwa kuwa wabunifu na mapenzi hayatawezekanika iwapo upande mmoja pekee ukiwa unajitahidi wakati mwingine unategea na kutokujali, na kila mkiongea hakikisha hamtumii sana neno nimekumisi, chochote kikiwa kinatamkwa sana na kusikiwa kila siku hupoteza mvuto na kuwa neno la kawaida na kusababisha maongezi kuisha mapema.
  • Namba 4, Tambulishaneni kwa marafiki wapya na usiwe na wivu na marafiki wake wa kiume.
Kitu kimoja uhusiano wa mbali unachosababisha ni kutoa muda mwingi wa kutumia na marafiki, kazi yako kama mpenzi wake unatakiwa usionyeshe wivu wako maana utakuona humuamini na kusababisha asikushilikishe kwenye baadhi ya mambo mengine maana anajua iwapo akifanya hivyo hautohafiki na zaidi ya hapo itasababisha ugomvi ambao haupo na itamfanya pia na yeye kuwa na wasi wasi na wewe pia, kujiamini na kutomtilia mashaka mpenzi wako kunatengeneza hali ya kuaminiana na kusababisha uhusiano ujijenge katika hali nzuri ya amani na yenye msimamo zaidi.

Kutambulishana kwa marafiki wapya inawafanya muwe huru na kupata mengi ya kuongea. 
  • Namba 5, Ongeeni kwa kutumia njia za kuonana mara kwa mara.
Tumieni tekenelojia iliyopo kuongeza hamasa, mvuto na chachu ndani ya mapenzi yenu, kuonana ana kwa ana kwa kutumia njia za skype, google talk au kutumiana video kwenye whatsaap kunaleta hali ya uhalisia zaidi na kufanya kusimuliana kuhusu kitu cha kijinga rafiki yako alichokifanya au mfanyakazi mwenzio anavyokuboa kuwe na hali ya mawasiliano yenye mvuto zaidi.

Kuona tena tabasamu lake na jinsi uso wake unapotabasamu kulipua hisia zako maradufu na za kwake pia na kusababisha hamasa na hisia zilizosahaulika kurejea tena kwa mara nyingine.




Share:

Unampenda kimapenzi hautaki kumpoteza, ila humuelewi amebadilika.


"Je upo kwenye uhusiano wa mapenzi na mtu maalumu ambaye hutaki kumpoteza?, Je unapata hisia mbaya na unahisi kunakitu hakiko sawa maana kila ukitaka kumbusu mpenzi wako au kukaa nae muongee hana hisia tena kama alizokuanazo awali, kila kitu anakuwa na kisingizio na mizungusho mpaka unapata hisia labda kuna mtu mwingine katikati?".

 Nikitu gani unachokijua ambacho wanaume wanakifanya ila wanawake hawakifanyi?, unajua ni nini?, wanaume hupingana na hali halisi katika sehemu mbili za maisha yao, namba moja; huwa hawaulizi njia inaelekea wapi au mahali walipo pindi wapoteapo njia na namba mbili; huwa wanadhani wanawake wote hawaeleweki wala hawaendani nao.

Watu hawa kamwe huwa hawajiulizi kwanini baadhi ya wanaume wengine huwezi kukuta wamekataliwa na mwanamke au wameachwa na mwanamke, je inawezekana kwamba baadhi ya watu hufanya makosa kwenye mahusiano na makosa hayo hujirudia kutoka uhusiano mmoja kwenda mwingine?, au inawezekana kwamba uchaguzi wa wanawake katika wanaume si dhabiti?

Muongozo; 

Wanaume walio na mafanikio kwenye mapenzi huwa hivyo sio kwa sababu ya bahati, ila ni kutoka na kutumia kanuni za kuaminika na kuwa na mipango thabiti.

Kiumeni.com imekuandalia kanuni thabiti ambayo unatakiwa uifatilie vizuri na kuielewa maana ndo itakuwa nguzo kuu ya mafanikio katika mahusiano yako ya kimapenzi na kukufanyia mabadiliko makubwa ya utanashati.

Kanuni; Kuwa na chamgamoto. 

Hamasa au mvuto wa mwanamke kimapenzi ni kitu cha muhimu sana cha kuangalia iwe wakati unamtongoza mwanamke au uko naye tayari katika mahusiano, wakati unamtongoza hamasa inakuonyesha kiasi cha uhakika ulionao kukubaliwa au kukataliwa, na katika mahusiano huonyesha kiwango cha mvuto wa kimapenzi alichonacho mwanamke juu yako, hamasa hupungua na kuongezeka kutokana na jinsi wewe unavyoendesha mapenzi na mpenzi wako, kanuni kuu ya kuongeza hamasa ni jinsi unavyotoa changamoto kwa mwanamke.

Changamoto ni kitu ambacho wanawake wanakitaka na ndicho kitu pekee kitakachomfanya mwanamke akae kwa muda mrefu, tuchukulie mfano umekutana na msichana mpya na mnaanza kuongea, maongezi yanaendelea na yanazidi kuwa matamu, unaanza kumwelezea kuhusu maisha yako pamoja na mahusiano yako ya kimapenzi yaliyopita, na kumgusia juu ya wapenzi wako wa zamani na mahusiano yako kwa ujumla na kwa jinsi anavyokusikiliza unajua kabisa mpo ukurasa mmoja kwa mambo mengi mnayoyaongea, mpaka kufikia mwisho wa maongezi umeshamwambia kila kitu kuhusu wewe, kwa hio kwa hapo unakua umeshamaliza changamoto yeyote uliokuanayo.

Naposema umeshamaliza changamto namaanisha hutakiwi kuwa muwazi sana, kama kaka yangu Abel anavyosema "Ukiona maongezi yamekolea na anakuangalia kwa jicho la husuda, kinachofuatia ni kuaga ili umwache anakufikilia.

Haimaanishi unampenda kiasi gani, unachotakiwa kuangalia ni kiasi gani upendo wake unavyoongezeka kwako na jinsi anavyoanguka kwenye mapenzi yako, ongoza matendo yako na maongezi yako, hakikisha haumsimulii mambo yako yote, mwache mwenyewe atafute na kufungua kurasa moja hadi nyingine ya maisha yako, kuwa changamoto kwa kumpatia kitu kitakachomfanya akufikilie, mwanaume kiongozianatambua changamoto ni sehemu kubwa ya mahusiano ambayo kipindi hiki wengi huwa hawazingatii, kwahio kama upo kwenye mahusiano ila unaona msichana wako amebadilika inatokana na kushuka kwa hamasa yake kwako, na hamasa ikishuka sana, tukichukulia hamasa kwa asilimia 0 mpaka 100%, na ikawa imeshuka chini ya asilimia 40% atakua anakuona kama unamboa na ni kitu cha kawaida kwa wanawake maana wanahitaji changamoto kwa wakati wote, na ikishuka sana chini ya asilimia 30% lazima atataka muachane.

Kwahiyo unawezaje kuwa na changamoto muda wote? 

Unachotakiwa kufanya ni kufanya hamasa yake juu yako iwe katika kiwango cha juu muda wate na si vinginevyo, lazima uonyeshe kujiamini na kujiheshimu kwa hio usije pitiliza na kujinadi sana na kitu kimoja naomba ufahamu kujinadi ni kuzuri kwa yule mchekeshaji mwenye uelewa na ujuzi mkubwa na wanawake, na ameshakuwa na wanawake wengi na anachohitaji zaidi ni ngono pekee.

Jiongoze kama mwanaume kiongozi , namaanisha tunza hisia zako na hakikisha zipo chini ya muongozo wako, kama ulikua mtu wa kumuhitaji sana kila muda jaribu kumpa nafasi, kama shemeji yangu anavyosema "Huwezi kukitamani kitu mpaka kipotee", na si maanisha usionyeshe hisia zozote kama jiwe ila weka uwiano na hasa katika mitoko yako ya kwanza.

Kujiheshimu na kujithamini ni sehemu kubwa ya kujiamini, kujithamini ni nguvu chanya na itakupa mwongozo mzuri kwenye uhusiano, kama haujiamini kwanini mtu mwingine akuamini?, tuachane na yote hayo mwisho wa kina ni kwamba muonyeshe mpaka ulipo, ila sio kwa kumwambia.

Kuwa na maamuzi kwenye uhusiano na unatakiwa ufanye maamuzi ambayo na kwako pia yanakunufaisha, na kama unamaamuzi yote kwake basi rafiki hapo ni mteremko tu.

mwanaume kiongozi anajiamini na anajithamini kwa hali ya juu na kufanya maamuzi ndani ya mahusiano kwa umakini zaidi na saa zote anaziongoza hisia zake na kama ukifanya hivi sawa, huyo msichana atakupenda daima na labda ndo atakaevalishwa ile pete.




Share:

Diamond, Nandy Bampa to Bampa








Share:

Mwanaume Kiongozi anawavutia wanawake kama sumaku, unajua ni nani na anafanya nini na je wewe ni mmoja wao?



"Ni watulivu, wanajiamini, wakiingia sehemu kila mtu anasimamisha anachokifanya na kugundua uwepo wao, wakiongea watu wote wengine wanawasikiliza, wengine wanataka kukaa nao wawasikie kile wanachozungumzia na kufanya, wanawake wanataka kutoka nao, hawa ni wanaume viongozi."

Mwanaume kiongozi anasifa moja ambayo inamtofautisha na mwanaume yeyote yule wa kawaida, yeye ni kiongozi asilia, mkusanyiko wa wanaume wengine unamfata yeye, anaongoza na kuwalinda wote wanaomzunguka.

Dunia ya mabadiliko inampa fursa nyingi mwanaumehuyu kiongozi, wakati wengine wanaona tatizo, mwanaume kiongozi katika asilia yake anaona sababu na athari, na anazibadilisha na kutengeneza fursa kwa jamii imzungukayo, anapenda kushinda na siku zote ndivyo alivyo.

Haupi kipaumbele muonekano wake, anachojari ni kushinda na kufanikiwa kwa kile anachokifanya kwa wakati huo, chochote anachokifanya watu wengine wanamfuata, wengine wanataka wafanane nae, wananakiri mitindo yake, jinsi anavyoongea na muonekano wake, mwanaume kiongozi yeye hufuata mitindo yake mwenyewe na hawezi nakili toka kwa mtu yeyote mwingine.

Mara nyingi anakua ametulia mpaka anapohitajika kufanya jambo, haogopi kupigania kwa kile kinachohitajika na chenye umuhimu na ni kiongozi mzuri wa wanaume aliyepo.

Kuna vitu ambavyo mwanaume kiongozi huwezi kukuta anafanya, Kiumeni.com imejaribu kukusanyia vitu kumi ambavyo iwapo na kama unavifanya basi ni dhahiri wewe sio mwanaume kiongozi.

            #10; Unamwachia msichana wako alipie gharama za mtoko.

Mwanaume kiongozi huudumia jopo lake na anawajibika kwa kila kitu, kama mwanamke wake akijitolea kulipa bili, ataichukua bili taratibu na kwa utulivu na kumwambia "niachie mimi", mwisho wa mjadiliano.

               #9; Hauombi msamaha hata kama umekosea.

Mwanaume kiongozi hakatishwi kitu, atasema kwa urahisi "Nimekosea nisamehe kwa hilo", na anasawazisha tatizo kama linawezekana.
              #8; Unajipendekeza kwa viongozi na kutafuta idhini yao.

Mwanaume kiongozi hajipendekezi kwa mtu, anajiamini na kuamini afanyacho maana yeye ni kiongozi asilia.

              #7; Unafanya Umbea.

Unafanya umbea juu ya bosi wako, rafiki zako na wengineo, haujali kuwasonta vidole watu wengine kwa mapungufu na udhaifu wao huku ukichekelea, mwanaume kiongozi hageuzii mgongo wenzake, anawasimamia na kuwaelekeza jinsi ya kufanya mambo na haitaji kujijenga kwa kuwaangusha watu wengine.
              #6; Unashituka kwenye majanga na haujiamini.

Mwanaume kiongozi asili yake ni mabadiliko na kujiamini, na mabadiliko ya kasi ni changamoto nzuri kwake, anapiga hesabu kwa kuangalia sababu na athari na majibu anayoyapata yanampa fursa ya kufanya kitu endelevu na cha muhimu kimaendeleo.
             #5; Unafanya mambo bila kufikiri.

Mwanaume kiongozi anafanya mambo kwa kasi, ila anafikilia kwanza kwa umakini mkubwa kabla ya kufanya, hakimbii ovyo ovyo na kukurupuka ila anatumia busara na umakini.
              #4; Unatoa lawama kwa wengine.

Mwanaume kiongozi anawajibika kwa matendo anayoyafanya.
               #3; Unadangaya.

Unadanganya watu wanaokuzunguka, unamdanganya bosi wako, unadanganya rafiki zako, mwanaume kiongozi sio muongo na anasimamia kile anachoongea na kama ni kitu kimeharibika anawajibika na kufanya kile kilicho sawa.
                #2; Unawasaliti wengine ili ufanikiwe.

Mwanaume kiongozi hasaliti watu wake, kama kuna kitu kinamtatiza anamfata mtu anayehusika.

               #1; Unawaonea wengine.

Mwanaume kiongozi hupigana pale panapohitajika na penye umuhimu wa kufanya hivyo, hapaparuki na wala kamwe hakurupuki na sio muonevu bali husaidia na kama kunatatizo hulitatua kwa kuwashilikisha wengine pale panapohitajika msaada.




Share:

Chameleone Afunguka Harmonize Kufuta Sauti Yake, ‘Sipendi Kukosewa Heshima’








Share:

Wakazi, Nikki wafunguka kuhusu Majani na Pro. Jay








Share:

Umeshamboa na kumuuzi Mpenzi wako, Tumia Njia Nzuri ya Kumuomba Msamaha.



"Hakuna kitu hawa watu wa jinsia tofauti wanachokijua kama kununa, na kama upo kwenye uhusiano wa kimapenzi lazima siku ifike mwenzio anapokataa kuongea nawe, inawezekana kosa likawa dogo au kubwa, hata kama hujui ni nini kimesababisha hawa viumbe ndivyo walivyoumbwa, kwao lazima kuna kitu utakosea tu, uwe umemtukana bibi yake au hujamsalimia mama yake lazima tatizo litakukumba tu ."

Jopo la Kiumeni.com baada ya kukaa na kufanya utafiti wa kina kwa marefu na mapana limekuandalia njia sita ambazo zitakufanya haya matatizo yasikuumize na kukusumbua sana moyo, njia hizi mbadala zitahitaji juhudi zaidi kutoka kwako na pia itakubidi uwe mbunifu kidogo na saa nyingine itakubidi umeze mate, uvute pumzi na kujifunga kiuwanaume na kitanashati na kukubali ya kuwa umekosea.

          #1; Tengeneza hali ya kimaongezi.

Utajua amekununia ikiwa kila ukimsemesha hataki kuongea nawe na kamwe huwezi kuyamaliza matatizo mpaka pale atakapoanza kuongea nawe na kukitoa kile kinachomuumiza moyo, kwa hiyo tengeneza hali ya kimaongezi ili aweze kukiongelea kile kinachomsibu mpaka kuwa hivyo na kukununia, using'ang'anize neno kwa kumuuliza mfululizo ni tatizo gani linalomsibu, kurudia rudia swali ni kusababisha makubwa zaidi.

Kama hujui kweli chochote kinachomfanya awe hivyo, jaribu kupatishia hata kama ukipatishia ambacho sio itasaidia maana utakua umetengeneza hali ya kimaongezi itakayofanya nyie wawili muweze kuongea tena.


          #2; Mfanye acheke na kutabasamu.

Ukiwa na uwezo wa kumchekesha ni kipaji kizuri kitakachoweza kukufikisha mbali na wanawake, japo sio kila muda kumfanya arudishe tabasamu kunawezekana, saa nyingine kunaweza kukufanya uonekane wa ajabu na kulipua hasira yake zaidi, kwahiyo kama ameuzika kwa hali ya juu, kumtania kutaongeza matatizo mara mbili zaidi na kuona kama unamchukulia ki mzaha sana.

Unatakiwa kupima hali halisi, kama kosa lako ni kusahau kuendea maziwa dukani kama ulivyokua umemuahidi, ucheshi kidogo unaweza kumaliza tatizo, na iwapo kosa ni kuwa amekukuta na alama ya lipstiki kwenye shati lako la kazini lile jeupe, hapo kijana usiingize utani hata kidogo.

          #3; Mnunulie maua ukiambatanisha chokuleti na kadi.

Kumnunulia zawadi ni njia rahisi nzuri kuondoa mnuno wake.
Ushauri; Kumtumia maua au zawadi baada tu ya kumuuzi kunapoteza uzito, anaweza kukudhania unajaribu kumnunua kwa zawadi wakati unajua ulichokifanya kimemuuiza hisia zake.

Ili uweze kudhibiti hii hali, mtumie zawadi baada ya kuwa umeshazungumza naye na kuweka mambo kidogo katika hali nzuri, na itaongeza chachu nzuri zaidi maana hata kuwa anategemea kitu kama hicho kutoka kwako na kufanya aongeze hamasa zaidi juu yako.
Ukimtuia kazini kwake ni vizuri zaidi maana atapewa sifa na wafanyakazi wenzake na kukufanya uwekwe juu zaidi.

          #4; Msikilize kile anachokiongea.

Mara nyingi wanawake wanapenda kutoa hasira zao kwa kuongea, anataka kujua kuhusu tabia yako mbaya iliyomchukiza na kwanini imetokea hivyo, na unaweza kuta ni kitu kidogo tu, labda wewe hukumsikiliza vizuri na ndo kimesababisha mambo yote haya kutokea.

Kusikiliza ni karama, mwache aongee na hakikisha upo makini wakati unamsikiliza na ni vizuri ukamwacha aongee bila wewe kuingilia kati kwenye maongezi, kumuingilia wakati anaongea ili kujitetea kutasababisha zogo na kufanya tatizo lipanuke zaidi.

          #5; Ondoka.

Saa nyingine kitu cha msingi unachoweza fanya ni kuondoka, toka nje ya chumba au nyumba, mpe nafasi apumue hasira zishuke, ni mwiko na usijaribu kuondoka wakati bado anaongea, ukishatambua yupo kwenye hasira kubwa sana haja ya kuendelea kuongea naye haito saidia, kwa muda huo ni vizuri kumwambia kuwa unampa nafasi apunguze hasira na kuweka mawazo yake vizuri ili baadae muweze kuongea mpate mwafaka na kuelewana vizuri zaidi, baada ya hapo unaweza kuondoka.


          #6; Omba msamaha.

Mwishoni hakuna kitu kinachoweza kufunika neno "Samahani" lililotoka moyoni, na huwezi kumaliza ugomvi naye iwapo usipolitumia.

Hakikisha wakati unaliongea unalimaanisha, mwangalie machoni kwa upole na sema "SAMAHANI", usiseme naomba msamaha wala samahani matendo yangu yamekuudhi, maelezo kama hayo hufanya maongezi kuhusu hilo jambo yaendelee zaidi, sema samahani na maanisha kweli baada ya hapo bainisha samahani yako ni ya sababu gani ili aelewe umeelewa kwanini ulikua umemuudhi, kama ulikua ni uhusiano wa muda mrefu, mkumbushe mlikotoka.




Share:

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger