juu

Saturday 31 August 2019

Anakupenda kweli kwa mapenzi ya kweli au ni swaga za kadi yako ya benki na pesa zako tu?


"Anajua kukutumia, anajua kukushika vilivyo kihisia za mapenzi na anajua kukukamatilia vilivyo!, ila gharama alizonazo zinazidi bajeti ya serikali!."
 Tuseme kwenye muda maisha yako yana kila kitu kinaenda sawa, unasehemu nzuri ya kuishi, unava vizuri, maisha yako yanaenda sawa na una uwezo wa kujipatia chochote kile unachohitaji.
Sasa hivi umejipatia mchumba ila kila saa swali hili linakuingia akilini "Je ananipenda mie kama mie au anapenda pesa zangu?".
Hizi hapa ni dalili ambazo kiumeni.com imekukusanyia ili kujua iwapo msichana uliyenae anakupenda kweli au anachokifuata ni ujazo wa pochi yako na hela zako, misho wa siku akuache solemba na kukuumiza roho yako.
  • Anataka zawadi za thamani...
Ukiwa unampa zawadi za kihisia ambazo hazina gharama zozote, ila zina kumbukumbu flani ambayo ni spesho kwenu, kumbukumbu nzuri ya wakati flani katika mapenzi yenu atakuangalia kwa jicho baya huku akielekeza pua yake kwenye zawadi anayoitaka.
Wanawake waliopo kwa ajiri ya pesa huwa hawana hisia na zawadi zenye umaalumu wa kipekee kwenye mahusiano ila wanapendelea zawadi zilizopikiwa gharama na fedha.
  • Marafiki zake wanaishi maisha ya gharama ya juu...
Kuna usemi usemao, "Utamjua mtu kutokana na iana ya marafiki waliomzunguka", kama msichana wako anatumia muda mwingi na marafiki wenye matumizi ya hali ya juu, ujue yupo nawe ili apate hio hela ya kukidhi garama ya hayo matumizi anayoyataka.
  • Ana hamasa kubwa ya kujua hali ya maisha yako kiuchumi...
Msichana wako anakua anakuuliza sana maswali ya hapa na pale yenye marengo ya kujua hali yako kiuchumi tokea siku ya kwanza upo nae, unaweza kuchanganya maswali yake na kudhani anataka tu kujua mambo kuhusu wewe kimaisha, hapa anataka kujua kama una uwezo wa kutosha wa kutimiza mahitaji yake katika kipindi chote cha mahusiano yenu.
  • Halipii bili hata siku moja...
Bili ikija mezani utamuona anakua bize na simu au kitu chochote kingine, anakua hata haioni kama ipo pale, hawezi kujitolea hata siku moja kulipia hata soda, ukiona hivyo ujue kakupenda kwa uwezo wako ulionao na sio kitu kingine.
  • Hajiamini mbele ya wanawake wengine wenye hadhi aliyojiwekea...
Siku zote anavaa vizuri kwa nguo za gharama, vito vya thamani na aliyependeza, na anafanya vyote hivyo kwa kutumia pochi yako, na kwa sababu kawekeza sana kwenye muonekano wake hapendi wanawake wengine wanaomfanana au wenye hadhi ya juu kumshinda yeye, saa zote anakua hajiamini wakiwepo karibu.
  • Anatumia maumbile yake na muonekano wake kupata mahitaji yake...
Atafanya chochote na kutafuta udhaifu wako kwake na ana uwezo mkubwa na ukufunzi mzuri juu ya mapenzi na anajua kuutumia vilivyo kukutoa hela na anaweza fanya hivyo katikati ya kufanya mapenzi au baada kukwambia baadhi ya mahitaji yake na shida zake. 
  • Anaangalia sana hadhi...
Anatunza hadhi yake saa zote na anahakikisha inabaki pale pale kwa nguo na vito vya thamani anavyovaa, huwa hapendi kuwa karibu na watu anaohisi wana hadhi ya chini na hutumia kiburi chake na maneno ya kejeri kuhakikisha wanakaa mbali nae.
Anaonyesha kupendezwa zaidi mwanaume anapoongelea maswala ya kifedha kuliko kitu chochote kingine.
  • Anawapanda wapenzi wake...
Badala ya kupanda cheo, anawapanda wapenzi wake, ukiangalia historia yake ya mahusiano kati ya mpenzi wake aliyopita na wa sasa, wa sasa anakua na pesa nyingi kuliko yule wa zamani, anafanya hivi ili kukidhi mahitaji yake ambayo yanakua yanapanda zaidi.
  • Yupo nje ya ligi yako...
Ukimwona unajua kabisa kutokana na jinsi alivyo kwa muonekano wake ya kuwa yupo nje ya ligi yako, ukimwangalia anakila kitu kizuri, na unaweza kujiuliza anatafuta nini na mwanaume wa aina yako. 
Ukiwa na pesa nzuri ujue yupo kuongezea zaidi hadi aliyoifikia kutoka kwako.
  • Anahadhi ya kuwa na cheo...
Ukimwona unaweza sema anafanya kazi sehemu flani ila sio kiivyo!, yeye yupo bize na starehe na kula bata kwa wingi, zaidi ya hapo hana kitu anachofanya ila gharama zake ni za juu kushinda uwezo wa kipato chake na anaujuzi mkubwa wa kutumia hisia zako kulipia kila kitu anachohitaji.




Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger