juu

Saturday 31 August 2019

Kim Nana Afunguka “Mimi Sijaachika na Wala Siwezi Achika Kirahisi Hivyo”

WALE mnaopenda kufuatilia maisha ya watu mpo? Haya sasa muuza nyago maarufu Bongo Lilian Kessy ‘Kim Nana’ amesema kuwa yeye kuachika siyo rahisi kama watu wanavyodhani au wanavyoomba iwe kila siku anajiamini ni msichana mzuri.

Kim Nana aliiambia Mikito Nusunusu kuwa mikwaruzano katika uhusiano lazima itokee hivyo hata yeye ametofautiana kidogo tu na mpenzi wake Tonny Albert ’T Bway’ lakini siyo kama wameachana kama ambavyo watu wanazusha na kibaya zaidi ni kwamba asilimia kubwa ya watu wanapenda kusema mambo ambayo hawana uhakika nayo.

 “Jamani eti nimeachika na kipigo juu, mimi siwezi kuachika kirahisi hivyo kama wanavyofikiria najiamini sana, sasa watu wanapenda kuongeaongea tu mambo wasiyokuwa na uhakika nayo.“Kutofautiana katika uhusiano ni jambo la kawaida sana tu, kwa sababu hata hao wanaoongea kuhusu mimi huwa wanagombana na watu wao wakaribu,” alisema.Nana haachiki kirahisi.










Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger