juu

Friday 30 August 2019

Poshy: Sitaki Mahari Kubwa Baadaye Isije Kutumika Kama Fimbo

MREMBO mwenye umbo matata Bongo, Jacqueline Obeid ‘Poshy Queen’ amesema pindi utakapofika wakati wa kuolewa, hataki mahari kubwa ili baadaye isije kutumika kama fimbo ya kumchapia.

Akizungumza na Amani, Poshy alisema watu wengi wanafikiri msichana ukitolewa mahari kubwa ni sifa kumbe ni kujitengenezea wakati mgumu mbele ya safari kwa mwanaume kukutumikisha akiamini amekununua kama bidhaa.

“Kama nina mtu wangu nampenda na yeye ananipenda kwa nini tusikubaliane tu wazazi wakatutambua, na ikifika hatua ya kufunga ndoa mahari yangu nataka bei ya kawaida tu maana wengine hata elfu thelathini anaolewa na anaishi vizuri lakini sio kila kukicha mtu anakufanyia vitendo vibaya ndani ukimuuliza anakuambia kakutolea mahari kubwa, mimi hiyo sitaki hata elfu hamsini naolewa tu,” alisema Poshy.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger