Kula vizuriKufanya mazoeziKupata usingizi wa kutoshaKuhakikisha umepata chanjo zote muhimu kwa ajili ya maradhi ambukiziTumia kinga (condom) kama hamfahamu hali zenu (Katika hili, thehabari tunashauri kama wewe ni mume, basi tafuta mke wa kuoa, na kama wewe ni mke, basi tafuta mume. Baada ya hapo, tulia katika ndoa yako, michepuko sio dili!!!)
Pamoja na kwamba kufanya mazoezi imetajwa kama nyongeza ya tendo la kujamiina kama vitu ambavyo vinaongeza vurutubisho vya kupambana na maradhi mwilini, tendo la kujamiina peke yake linahesabika kama mazoezi. Ndio maana, faida kuu ya pili ni kukufanya ufungue gym kitandani. Kwa maneno mengine, kujamiiana ni njia moja wapo ya mazoezi. Hapa ni muhimu kukumbuka kwamba hata mazoezi yanahitaji mapumziko, kwahiyo usije ukafanya tendo hilo kutwa nzima (kama unao ubavu) na kutegemea faida, badala yake utachuma hasara, ambazo sio mjadala wetu leo. Kama tendo hili litafanyika kwa umakini na utaratibu maalum, basi wataalam wanasema tendo hilo linachoma kalori (calories) tano kwa dakika, kalori nne zaidi zinachomwa ukilinganisha na mtu anayeangalia TV!
Wanandoa wakiwa katika miondoko kama walivyonaswa na kamera ya thehabari
Sababu kuu ya tatu, tendo la kujamiiana linapunguza uwezekano wa kuvamiwa na mshtuko wa moyo (heart attack!). Ukiachilia mbali kwamba tendo hili ni njia nzuri ya kuongeza mapigo yako ya moyo, pia ni njia nzuri ya kuhakikisha viwango vyako vya estrogen na testosterone vipo katika mizani sahihi kitu ambacho ni muhimu linapokuja suala la kuzuia uwezako wa kupatwa na mshtuko wa moyo, wataalam wanamalizia.
Hizi ni baadhi tu ya faida, bila shaka unazifaham faida nyingine lukuki, ambazo hazikutajwa hapa. Kama tulivyoonya hapo juu, kujamiiana ni tendo la kiungwana na lina faida nyingi kwa afya yako, hivyo basi, tafuta mke au mume, halafu dili nae! Michepuko sio diliii!
source https://sirinzitozamapenzi.blogspot.com/2019/08/faida-tatu-za-tendo-la-ndoa.html
0 comments:
Post a Comment