juu

Saturday 30 November 2019

Jinsi Ya Kumsisimua Mwanamke Kabla Ya Kulala Naye

Related image
Unapaswa kumsisimua kuanzia nafasi ya kwanza ambayo utaipata kutoka kwake. Kufanya hivyo kutamfanya akutake hata zaidi na kumfanya ajiandae na mapema kabla hata kulala naye. Lakini ni mbinu gani inayoweza kutumika kumsisimua mwanamke kabla hamjalala pamoja?

Zama nami…

Kutumia maneno
Maneno yanaweza kumsisimua mwanamke asilimia mia. Mwanzo wanawake husisimuliwa na vitu wanavyosikia zaidi kuliko wanavyoona. Hii ndio tofauti kuu kati ya jinsi ya kumsisimua mwanaume na mwanamke. Hauhitaji kuonekana mchafu wakati ambapo unamsisimua mwanamke kwa kutumia maneno. Mwanzo anaweza kusisimulika na jinsi ambavyo anakusisimua wewe. Unaweza kumwambia maneno kama “Siwezi kungojea ile siku ambayo nitakuwa pekeangu na wewe”, “Nimeanza kuingiwa na mawazo nikifikiria hio nguo uliyovaa inaficha nini” ama maneno mfanano na haya.

Lakini kando na kuwa maneno yanamsisimua mwanamke, kutategemea pia na vile ambavyo unamshika na miguso yako.

Kutumia miguso
Hapa ndipo utaleta utofauti wa yote. Miguso ni mbinu nzito na ya nguvu kama unaazimia kumfanya akutamani, kabla hata nguo za yeyote kuvuliwa, kabla ya nyinyi wawili kuanza kubusiana ama kufanya chochote. Baadhi ya mifano ya kufuata ya kumsisimua mwanamke kwa miguso ili aweze kukutamani kabla ya nyinyi wawili kulala pamoja ni kama ifuatayo: [Soma: Hatua za kumfanya mwanamke awe huru unapomgusa]

Kuzivuta nywele zake kiulaini: Usizivute nywele zake hadi ukazing’oa kichwani mwake. Lakini usiogope kuzishika baadhi ya nywele zake na kuzichezea kimvuto.

Miguso ya kukawia: Wakati ambapo unamgusa kikawaida – kwa mfano, wakati mikono yako iko katika mabega yake, mgongo au mkono – usiogope kuuzuia mkono wako ukawie sehemu hizo kwa dakika moja.

Karibu kumla dende: Hii ni siri kubwa ambayo inahakikisha gemu yako kuwa ya juu. Usikimbilie kumbusu. Jiweke katika hali ambayo nyinyi wawili mko “karibu” kubusiana. Hii itamfanya aingiwe na wazimu wa kutaka kuibusu midomo yako haraka kuliko ulivyokuwa ukitarajia.

Kumkwaruza kiulaini: Unapomgusa, usiogope kuzipitisha kucha zako kwa mgongo wake, nyuma ya shingo yake na sehemu mfanano na hizi. Hii unaweza kuitumia wakati ambapo mshajenga uhusiano wa ndani kati yenu.

Mtizamo wa macho: Kumuangalia mwanamke kwa macho pekee kunaweza kumfanya apandwe na mzuka. Mwangalie machoni, zaidi kuliko yeye. Kufanya hivyo kunaashiria ujiaminifu. Ijapokuwa mbinu hii haitumii miguso, inaweza kufanya kazi sawa na kama vile matumizi ya miguso kabla nyinyi wawili kulala pamoja.

Ok hizi ni baadhi ya mbinu za kumfanya mwanamke asisimke kabla kulala na yeye
Share:

Ili Mpini usimame vizuri ni lazima:πŸ”₯ πŸ”₯

Image result for kumsifu mpenzi wako asikuache
Mfumo wako wa neva uwe na afya nzuri inayopelekea mpwito neva (nerve impulses) katika ubongo, uti wa mgongo na uume.
Mishipa ya ateri iliyo na afya ya ndani na iliyo karibu na corpora cavernosa
Misuli laini yenye afya na tishu za ufumwele (fibrous tissues) ndani ya corpora cavernosa
Kiwango sahihi cha oksidi nitriki (nitric oxide) ndani ya uume.

Uume kushindwa kusimama vizuri kunaweza kusababishwa pia kama kipengele kimojawapo hapo juu hakifanyi kazi vizuri.
Mambo mengine yanayopelekea kupunguwa kwa nguvu za kiume, uume kushindwa kusimama vizuri na kuwahi kufika kileleni ni:
Uzee
Kisukari
Kujichua/Punyeto
Uzinzi
Kukosa Elimu ya vyakula
Kutokujishughulisha na mazoezi
Shinikizo la juu la damu
Ugonjwa wa moyo
Uvutaji sigara/tumbaku
Utumiaji uliozidi wa kafeina
Kudhurika kwa neva au uti wa mgongo
Madawa ya kulevya
Kupungua kwa homoni ya testerone
Athari kutoka kwa baadhi ya dawa
Pombe
Kutazama picha za X mara kwa mara
Share:

Mambo muhimu ambayo ukimfanyia mpenzi wako yatazidisha mapenzi na kuongeza furah





katika Mapenzi kuna vitu vingi unaweza kumfanyia Mpenzi wako ukamfurahisha na kumfanya azidishe Mapenzi ila katika safu hii nitazungumzia Mambo machache muhimu yatakayokusaidia kuboresha na kudumisha penzi lako kwa umpendae KARIBU:
YAFUATAYO NI MAMBO MUHIMU YANAYOZIDISHA
UPENDO:

1.KUMNUNULIA ZAWADI MPENZI WAKO:
» Zawadi ni moja ya sehemu husika katika Mapenzi inayoweza kufanya penzi likawa bora na lenye kupendeza siku zote, faham kwamba hakuna mtu asiependa kupewa zawadi na kila anaepewa zawadi siku zote hujihisi kama ni mtu anaependwa na anaejaliwa na

kuthaminiwa hususani katika ulimwengu wa Mapenzi unapompa mpenzi wako zawadi basi faham ya kwamba utamfanya mpenzi wako ajione kama ni wapekee kwako na anathamani kubwa kwako hivyo hatosita kudhihirisha mapenzi yake kwako, kikubwa zingatia pindi unaponunua zawadi kwa ajili ya kumpa mpenzi wako jitahidi kuwa mbunifu na uwe ni mwenye kubadilika sio kila siku zawadi zile zile zinajirudia kwa kufanya hivi utamboa mpenzi wako kuwa mbunifu na jaribu kumpa mpenzi wako zawadi zenye kutunzika mfano kama Card, maua, nguo n.k. Utamfanya azidi kukupenda zaidi na zaidi.

2. MSIFIE MPENZI WAKO:
» Sifa zinaleta changamoto katika mapenzi. Unapaswa kutambua kuwa usiwe mchoyo wa sifa kwa mpenzi wako usisubiri watu wapembeni wamsifie mpenzi wako pindi anapofanya jambo zuri na lenye kupendeza chukua nafasi hii wewe kama kioo chake unadhani usipo msifia mwenza wako unataka nani amsifie?! Jitahidi kudhihirisha sifa kwa mpenzi wako kwa mfano umemuona mpenzi wako kapendeza basi usisite kumwambia “Sweetie nimependa vazi lako la leo ama hakika umetoka sex nakutamani zaidi ya siku zote navyokutamani ingawa siku zote unaziteka hisia zangu ila leo ni zaidi” unaweza kumpa maneno kama haya na mengine mazuri ya kuvutia, sifa zipo nyingi mbali na kumsifu mavazi yake hata tabia n.k. Kwa kufanya hivi utamfanya mpenzi wako azidishe mapenzi kwako kwani atahisi kampata mtu anaejali ubora na uhalisia wake kimaumbile na kimatendo. ZINGATIA:- Usitoe sifa ilimradi sifa zisizo na ukweli.

3. EPUKA KUMUUDHI MPENZI WAKO:
» Sote tunafahamu kuwa hakuna binadamu aliekamilika na hakuna alietolewa nyongo kila mtu anakasirika na anakosea ila solution kubwa ni kudhibiti hasira na kurekebisha makosa na kusuluhisha hususani kwenye mapenzi, katika mapenzi hakuna jambo baya linalopunguza upendo kama ugomvi na kumuudhi mpenzi wako mara kwa mara. Ili kuboresha mapenzi na kulifanya penzi lako liwe imara na lenye kuvutia basi jitahidi kuepuka kumuudhi mpenzi wako na pindi ikitokea umekorofishana na mpenzi wako jaribu kutafuta suluhu mwite kaa nae muombe samahani iwapo kama unakosa na hata ikitokea kosa si lako pengine kakuudhi na bado unamuhitaji usikae na kinyongo wala usiumize nafsi yako kaeni muyamalize muendeleze mahusiano yenu na msiwe watu wa kuzungumzia tofauti zenu kwa watu wa pembeni.
Kwa kufanya hivi daima mtakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na mapenzi yenu hayatofika kikomo zaidi yataendelea kushamiri.

4. MFANYIE YATAKAYO MFURAHISHA:
» Kuna mambo mengi mazuri na yakuvutia katika mapenzi unaweza kuyafanya kwa mpenzi wako yakamfurahisha kwa mfano unaweza kusoma tabia ya mpenzi wako na ukajua ni nini anapenda na kipi hapendi kufanyiwa ukajitahidi kujilinda kumtendea asiyoyapenda na ukaufungua moyo wako kwa kumridhisha kumfanyia kile anachokipenda. Katika mapenzi watu wengi hupenda kutolewa Out, kupewa ofa ya lanch, kupewa zawadi zenye mvuto na zenye hamasa nzuri kwenye mapenzi. Unaweza kufanya vitu vizuri vyenye kuvutia kwa mpenzi wako vikamvutia ikawa ni nafasi nzuri kwako kumfanya azidishe mapenzi.

5. KUWA MTU WA UTANI KWAKE:
» mpenzi msomaji ninapozingumzia mapenzi na maanisha mazoea yaliyoambatana na upendo, siku zote mapenzi hujijenga moyoni kwa mtu kutokana na ukaribu na mazoea yaliyopo baina ya watu wawili, katika pointi hii ya mwisho nataka nizungumzie utani katika mapenzi unafaida gani. Mpenzi msomaji fahamu yakuwa utani ni moja ya sehemu katika mapenzi na utani unasaidia kuboresha mapenzi ila utani ninaotaka kuuzungumzia hapa ni utani wa kawaida na sio ule wa kuvuka mipaka. Elewa wazi kabisa unapokuwa

na mpenzi wako na ukawa ni mtu wa utani inakusaidia wewe kumfanya mpenzi wako akuzoee na awe anajisikia kuwa karibu nawewe muda wote kwani utakuwa unamfurahisha kutokana na utani wako.
ZINGATIA:- Usivuke mipaka ya utani, usimtanie kupitiliza, mtanie kutokana na mazingira, usiwe utani unaofanana nakweli, mtanie kwa faida.
Share:

Jinsi gani ya kuongea na msichana bila kupungukiwa Swaga




Jifunze jinsi ya kuongea na msichana bila kupungukiwa na swaga, bila ya kujali upo wapi. Unachohitaji ni hivi vitu 10 hapa kufanya maajabu na kumteka!.
Mfate alipo

Moja ya vitu ambavyo ni vigumu kwa wanaume wengi kufanya ni kumfata msichana anayemtaka kwa mara ya kwanza.

Kuchati na mwanamke ni kitu rahisi sana hatakama hamkuwahi kuonana, lakini kumfata ndipo kwenye utata.

Wakati unapohitaji kumfata msichana ambaye haukuwahi kuongea nae kabla, na ukahitaji kuanzisha maongezi, moyo huanza kwenda kasi kama ngo'ombe anayekwenda machinjoni.


Fata hizi hatua 10 kwa uda huu mfupi, na kabla haujafika huko, kujua jinsi ya kuongea na mwanamke unayemtaka itakua rahisi kama vile mtu anayetembea kwenye bustani.
Unapenda sana kuongea na wanawake wa hadhi(high status), si ndiyo?
Kama vile upendavyo, vivyo hivyo wanawake hupenda kuongea na wanaume wa
viwango.
Kwa maana hiyo, hakuna cha kuogopa hapa!.
Kumbuka, sheria kubwa ya kuijua wakati unataka kujua jinsi ya kuongea na mwanamke unayemtaka - hautakiwi kuvuka hatua. Kama ulivyojifunzaga kutembea kabla haujajua kukimbia, unatakiwa kujua jinsi ya kumtamanisha hata kabla haujaongea nae.

Sasa Twende..

# 1Mfanye ajue kuwa unamtaka. Najua unajua, kuongea na mwanamke kwa mara ya kwanza siyo kama mtu anayemfata mwanamke na kumuomba watoke out. Inatakiwa iende kwa hatua, lakini licha ya hiyo hautafikia lengo. Mwanamke anahitaji kujua unamtamani/ kumpenda hata kabla hamjaongea ili aweze kukuchambua / kukufahamu / kukuchunguza(to evaluate you).

Kama utamfata mwanamke ambaye kwanza hajawahi hata kukuona ukionesha interest kwake, utaishia kumshtua tu. Na ataishia kukwambia neno ambalo mama yake alimfundisha akiwa mdogo - kwamba akikutana na mwanaume amwambie nini "Niache".

.

#2 Fanya mautundu. Baada ya kujua kuna kiumbe kama wewe duniani, anza michezo ya kichokozi. Jitahidi kuwa unamuangalia kila wakati mpaka yeye ajue unamuangalia, hii itamfanya naye awe anafanya hivyo hivyo japo hatapenda kujionesha(ila usimshangae). Sasa unatakiwa kujua, na yeye anakuangalia? je marafiki wake wanakuangalia? je wanatabasamu wakikuona?. Jaribu kujua hayo.


Hakuna haja ya kutaka kujua jinsi ya kumfata mwanamke ambaye ukimtazama anakuangalia vibaya au kwa hasira, na wakati mwingine hajali kama unamuangalia au la. Kumbuomba mwanamke kutoka nae mda mwingine huwa kama majanga kama haujamvutia, hivyo kuwa mwangalifu.

#3 Usimchomoe au kumuita kutoka mahali. Kumchomoa mwanamke kutoka sehemu fulani mara nyingine huwa smart na ya kuvutia, lakini mara nyingi siyo njia sahihi. Jitahidi kuangalia mazingira.
Mfano kama alikua sehemu fulani, kisha akawa anaondoka unaweza mfata na kusimama mbele yake na kumuabia vitu kama " natamani ungejua ni kwa muda gani nimekua nikitamani kuwa na muda kama huu". au kitu kingine cha kawaida. Iwe ofisini, park ya magari au hata bar, jaribu kumuuliza swali ambalo linaendana na mazingira.

Lakini kumbuka kutumia lugha ambayo itamchanganya ka kutaka wewe uongee zaidi ili akuelewe.

#4 Usikamie maongezi. Hii hufanikiwa vizuri pale unapomuuliza maswali ya kumchanganya na kuwa anakujibu. Akishakujibu, wote mnakua katika mood ya kuongea lakini bado hamjawa marafiki. Atakuwa anayajibu maswali yako huku akitazama sehemu nyingine. Wakati mwingine anaweza hisi unamtania au unataka kumchanganya, hivyo hatatamani kuendelea na maongezi

Unaweza ukafanya hivi, Jitambulishe wewe ni nani au endelea kumuuliza maswali kisha baadae kidogo jitambulishe. Kwa kuangalia muitikio wake wa maongezi, mwambie ni kwa muda gani umekua ukitamani ukutane nae.

Tayari anajua ni kwa muda gani umekua ukimtazama, kwa hiyo huna haja ya kuigiza kwamba umestukiza.


#5Mpe nafasi. Usimsimamishe maeneo ambayo yatamfanya asiwe anajiamini, mazingira kama vichochoroni au sehemu za kujificha. Kama utaweza, unaweza ukaongea nae hata mbele ya rafiki zake. Kumbuka, ukimsimamisha sehemu ambayo ni salama itamfanya ajisikie kujiamini na kukuamini pia kuwa wewe siyo mtu mbaya.

Baada ya kumchangamsha, sasa atakuwa anatamani aendelee kuongea na wewe zaidi na utazidi kumvutia kiasi kwamba hataweza kutambua kama unamtega ili uwe nae.

Bado tupo njiani, hatujafikia lengo la kuhakikisha swaga hazipungui. Ila hizi tips zinatosha kabisa kumvutia mwanamke na akaanza kuongea na wewe na kupenda kampani yako muda wote.
Sasa soma hizi tips nyingine 5 ujue ni kitu gani utaongea na huyo msichana ili uendelee kumtamanisha aendelee kuongea na wewe kwa vile unavomfurahisha moyo wak
Share:

SMS-TAMU-MPYA-ZA-MAHABA

Related imageT.gifSMS ya mapenzi ya mahaba kwa mpenzi wako aliyeko mbali

Kuna bahari kati yetu. Misitu na milima inatutenganisha,
mimi si ‘Supamani’ lakini nipe sekunde moja nitavuka nchi
nyingi kukutumia mapenzi yangu. Umeipata hiyo? Pokea mapenzi yangu japo uko mbali.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifUjumbe wa kimahaba wa kumtumia msichana umpendaye kumwambia kuwa utampenda daima

nashtumiwa kwa kumpenda mcchana mmoja aliyeutesa moyo
wangu
mahakama imenihukumu kifo kwa kunyongwa na kamba upendo
lkn kwa msamaha wa raisi mapenzi
nmehukumiwa kuwa mwaminif kwake nakumpenda zaidi ya hapo
daima milele.
nakupenda mpz

πŸ”₯♥♥♥


T.gifUjumbe mzuri wa mapenzi kwa umpendaye akupende zaidi

Moyo wng mtiifu,2li ume2a kwako,kwang huna upungufu yote nimekupa hekoo,utunze na ulee pia uujali kama mama yako alivyofanya kwako.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifUjumbe mzuri wa kumuomba mpenzi wako asikuache

Mapenzi ni matamu napia yana raha, wewe hauni ishi hamu, siku zote wanipa raha, wewe kwangu ni mtu muhimu, unaeng'aa moyoni mwangu kama nyota ya jaha. "NAKUOMBA USINIACHE MPENZI WANGU"

πŸ”₯♥♥♥


T.gifUjumbe wa kimahaba wa kumtumia mpenzi wako

Ikiwa penzi langu kwako litakufa halitazikwa,ikiwa moyo
wangu ni mwandiko hautafutika na kama dhati yangu ni
machozi daima hayatokauka na wewe kwangu ni damu ngozini
haitochuruzika ila mishipani… .

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS nzuri kwa mpenzi wako kumwambia kuwa ameitibu akili yako

Chuki huharibu akili; mapenzi huitibu. Umeitibu akili
yangu.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS ya kumtumia mpenzi wako aliyesahau kuwasiliana na wewe kumkumbusha awasiliane na wewe

Ni yangu mazoea kila cku cm yako
kuipokea kama si meseji
kunitumia
leo naumia kila napo fikiria nini
kimetokea hadi
mawasiliano yetu
yameanza kupotea,sawa tu.naamini hali
ya kawida itarejea
na
majonzi moyoni yatanipotea
nakupenda mpz

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS nzuri kwa ajili ya kumtumia mpenzi wako kumwambia sababu ya kumpenda

mapenzi ni safari,mapenzi ni ahadi,mapenzi ni
ujasiri,mapenzi ni zawadi,mapenzi mitihani,mapenzi
ramani,mapenzi ajali na ndiyo maana nakupenda wewe bila kujali.

πŸ”₯♥♥♥

Share:

Ukiona Dalili Hizi Ujue Mpenzi Wako Anachepuka




Mapenzi ni matamu lakini huingia shubiri pale mambo yanavyoenda mrama. Je umekaa kwenye uhusiano na mumeo/mkeo/ mpenzi wako kwa muda mrefu kwa raha na amani lakini ghafla unaanza kuona mambo yanabadilika?

Wanawake wengi na wanaume wengi hawataki kuamini yule umpendaye anaweza akachepuka lakini ndio hivyo wengi wao huishia kuwa wasaliti kwa wapeenzi wao.


Hizi ni dalili atakazo zionyesha mpenzi wako akiwa anachepuka:

1. Matumizi Makubwa Ya Mtandao wa kijamii

Kwa ulimwengu huu wa sayansi na teknologia na uwepo wa utandawazi simu za mkononi zinatumika sana kuficha maovu yaani ukishaona mpenzi wako anaweka na kubadilisha password kila siku, anatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii na kupendelea kuweka picha akkiwa peke yake na kusema kuwa hana mke au mume basi mchunguze vizuri mpenzi wako maana huwezi jua.

2. Atabali Muonekano wake au Mavazi

Ukikaa na mpenzi wako kwenye mahusiano kwa muda mrefu na umeshamzoea kwa kufanya vitu fulani au kuvaa mavazi fulani lakini ghafla unashangaa anabadilika anavaa tofauti anatumia muda mwingi kujibadilisha kama umri umeenda utaona anaanza kubadilisha mavazi ilimradi tu awe tofauti basi hutakuwa na jingine la kufanya zaidi ya kumuangalia mpenzi wako kwa karibu maana dalili zote zinaonyesha inawezekana anachepuka.

3. Mlalamishi/ Mrusha Lawama

Mtu yoyote anayefanya kosa basi ana kawaida ya kujishtukia hii inatokana na yeye kujisikia vibaya kwa vitendo anavyokufanyia kwaiyo ukiona mpenzi wako anaanza kukusingizia vitu kama vile kwa nini una ukaribu na marafiki zako wa jinsia tofauti na wewe basi jua wazi kabisa anafanya hivyo kwa sababu hivyo ndio vitu yeye anafanya.

4. Mawasiliano Yatapungua

Mkiwa kwenye mahusiano hakuna kitu cha muhimu kama mawasiliano kwani ndio kitu ambacho kitawafanya muwe karibu kwaiyo ukishaona mpenzi wako haongei na wewe mkikaa hamna cha kuongea au saa nyingine anaona hata mzigo kukaa chini na kuongea na wewe basi jua wazi kuwa mpenzi wako huyo anachepuka.

5. Kutumia Simu Kwa Siri

Simu za mkononi zinachukua nafasi kubwa katika kuharibu mahusiano ya watu ghafla utaona mkiwa pamoja simu yake anaweka mbali au hata ikiita mbele yako hawezi kupokea akaongea kwa uhuru hivyo ataenda kuongelea nje au hata chooni au hata akipokea mbele yako hatakuwa na uhuru. Mkiwa mbali ukipiga simu yake basi itakuwa inatumika maraa
Share:

Athari Za Mapenzi Mahala Pa Kazi



Endapo wewe unakuwa ni mfanyakazi basi sehemu kubwa ya maisha yako baada ya kuajiriwa itakuwa ni eneo lako la kazi, muda mwingi utakuwa ukikaa na wale wanaokuzunguka zaidi ofisini kuliko nyumbani.Kuna baadhi hata ya tabia zinaweza kuwa zinajulikana sana na wafanyakazi nwenzako kuliko hata familia yako, kitendo cha kuwa na muda mwingine na wafanyakazi wenzako kinaweza kukufanya uingie kwenye mtego wa kuanzisha mahusiano ya kimapenzi kazini ikiwa tayari ulishaoa au kuolewa au ndio unataka kuingia katika mahusiano.

Kwa kawaida kufanya kazi na mtu katika mazingira yaleyale ndio usababisha watu kupendana sana,wengi usema kuwa mapenzi katika mazingira ya kazi hayaepukiki,hii ni kweli kabisa kwa sababu muda mwingi mnakuwa pamoja.


Chukulia mfano unaondoka nyumban asubuhi sana na unarudi jioni sana, je utapata wapi muda wa kuonana na watu maeneo mengine, ukweli unakuja kwamba kumbe kazini ni moja ya sehemu inayoweza kukupa mpenzi wa kudumu.Lakini jitahidi kuwaza yafuatayo ukiwa unataka kuanzisha mahusiano hayo:
Ukaribu wenu unaweza kuwatenganisha na wengine

Ni vigumu kuficha hisia za mapenzi mbele za watu, mtajitahidi kuwa kimya ila kuna kipindi waliopo pembeni yenu wataanza kujua mahusiano yenu tu, na hapo ndipo zitaanza kutokea nyufa za matengano,kama mmoja wenu alifanya hivyo ili kupata mchepuko atakae mpa amani anapotoka katika mafarakano ya nyumbani basi mtaogopa habari kufikia mlengwa mmoja wapo, lakini pia mtakapokuwa mnasemwa ofisini mtahisi kama wenzenu wanawaonea wivu.

wapo watakaokuwa wanaheshimu hisia zenu na hata kuwa wanawapisha muwe na faragha na maongezi yenu, lakini kwenu inaweza kuwa ngumu kuelewa hivyo zaidi ya kuona kama manatengwa tu.
Mgongano wa kimaslahi.

Mapenzi yanaweza kuwa kikwazo katika utendaji kazi,ikiwa mmoja ni muajibikaji kwa mwingine na tayari mmeshaingiza swala la mapenzi katikati yenu itakuwa vigumu kutiliana mkazo au kuwajibishana kwa sababu tayari kuna mapenzi kati yenu.hali hii inaweza kukufanya ukawa mtoro, kuchukia kazi au kutokufanya kazi kwa umakini ukijua kuwa kuna mtu anaekukingia kifua eneo lako la kazi.
Ikitokea mkaachana.

Sio kila mahusiano yanadumu kama tunavyokuwa tunategemea pindi tunapoyaanzisha, hapana lakini ikitokea sasa mmeachana ni vigumu kuendelea kukaa sehemu moja na mtu ambae amekuwa akikujua kwa zaidi ya sana na bado mmegombana alafu mnakuwa mnapishana milangoni au kumtumiakia kwa kuwa inakubidi ufanye hivyo.
Upelekea kupoteza kazi.

Ikitokea mmeshagombana na mmekuwa maadui ni vigumu tena kuwa katika eneo moja hii itafanya mmoja wapo ambae hayupo huru kuondoka kutafuta amani yake,lakini pia endapo ikigundulika kuwa chanzo cha kutokuwa na ufanisi wa kazi kwa watu fulani ofisi unasababishwa na uhusiano wa kimapenzi uliojengeka baina yao basi ni rahisi mmoja kupoteza kazi au wote.
Share:

Umuhimu wa Tendio la Ndoa Kiafya



Wataalamu wanasema kuna umuhimu kubwa kwa mwanadamu kufanya tendo la ndoa kwa ajili ya kuimarisha afya yako,kwanza kabisa inapunguza mafuta mwili lakini pia inasemekana kuwa endapo mtu anafanya tendo la ndoa mara tau kwa wiki ndani ya mwaka mzima ni sawa na kukimbia maili75,tendo la ndoa uongeza vizalishi 150 katika mwili ambapo kwa nusu saa ni sawa na kukimbia dakika 15.Sio hayo tu umuhimu mkubwa wa tendo la ndoa unakuja katika yafuatayo’
kuongeza mwendo wa damu mwilini.

Tendo la ndoa uongeza kasi ya mtiririko wa damu katika mwili wa mwandamu, hasa katika ubongo na sehemu mbalimbali, lakini pia hii usaidia zaidi usaidia zaidi kasi ya mapigo ya moyo na katika mfumo wa upumuaji.

Msukumo mzuri wa damu mpya yenye oxygen husaidia zaidi katika uunguzaji mzuri wa chakula lakini pia ni vizuri kwa sababu usaidia kutoa uchafu katika mishipa ya damu ambayo ingeweza kumfanya mtu kuumwa mwili.
Kupunguza mafuta mwilini(cholestrol)

Tendo la ndoa uweka uwiano sawa kwa mafuat yenye kileo mwilini yaani kwa ile iliyo mbaya na hata ile iliyo nzuri uziweka sawa ili mwili ufanye kazi kwa uwiano sawa.
Kupunguza maumivu ya mwili

wakati wa tendo la ndoa homoni iitwayo oxytosin huzalishwa mwilini ambayo hii uchangia kwa kiasi kikubw akutengeneza kwa endorphini ambayo husaidia kupunguza maumivu ya mwili kama vile kuvimba sehemu mbalimbali za viungo(arthitis) , shingo (whiplash) na maumivu ya kichwa.
Kupunguza mfadhahiko ya moyo na kuondoa msongo wa mawazo.

Inaaminika kwamba mara nyingi watu wanaoshiriki tendo la ndoa mara kwa mara ni watu wenye tabasamua muda wote,hii ni kwa sababu mara mtu anapofanya tendo la ndoa na kupata muda wa kupumzik ahujikuta akijisikia vizuri na mwenye nguvu muda wote.wapo wachache waliowahi kuthibitisha kuwa wanapata usingizi mmno wanapomaliza kufanya tendo la ndoa na kulala,lakini pia wengi wamekuwa wakikiri kuwa siku zao huwa njema wanapopata muda wa kufanya tendo la ndoa asubui kabla ya kuingia katika kazi na majukumu mbalimbali.
Kuishi Muda mrefu huku ukionekana kijana.

Wakati wa kufanya mapenzi homoni iitwayo DHEA uzalishwa mwilini na kusababisha msisimuko katika mwili, homoni hii uwa na kzi kubwa ya kurekebisha mwili,kuongeza ufahamu,kumiarisha mifupa na kutengeneza afya ya moyo.
kuondoa baridi na mafua.

Elimu inaonyesha kuwa wanaofanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa chembe chembe hai za mwili kwa 30% , chembe hizo ulinda mwili kutopatwa na magonjwa.
Share:

Jinsi Unavyoweza Kujua Uko Kwenye Mahusiano Hatarishi.



Sio kweli kuwa watu wanaokaa muda mrefu katika mahusiano ndio wanaweza kukumbana na uhatari katika mahusiano , wapo ambao wamekuwa wakianzisha mahusiano kwa maslahi yao binafsi lakini wenzi wao wanapata tabu kujua kwa sababu wanakuwa tayari wameshapenda.

Hata kama mmekuwa na mahusiano kwa muda wa wiki moja tu, ni lazima kuwa mwangalifu na mtu unaeingia nae katika mahusiano ili kujua kama uko kwenye hatari ya kuumia kwa namba yoyote ile.



Watu wengi hawataki kuamini kuwa kule wanakopenda kunaweza kuwa na hatari ya kuumia , wengi wanaamini kuwa kama mtu anaweza kukuonyesha kukupenda hasa kwa maneno basi anakuwa tayari ameshachanganyikiwa na hakuna kitu unaweza kumwambia , lakini kumbe kuna mazingira yanaweza kuchunguzwa taratibu na ukagundua baadhi ya vitu kama.

Uthibiti usio wa kawaida (Over Control )

kuna watu katika mahusiano haoni kama mwenzake ana thamani kama inavyopaswa kuwa, yeye anataka kuwa muamuzi wa mwisho katika kila kitu, anataka awe msemaji wa mwisho kwa kila kitu, na kama utabisha basi mnaweza kukaa bila maongezi mpaka atakapojisikia kukusemesha wewe.Mfano yapo mahusiano ambayo , mmoja kati yenu anataka kuwa anajua kila kitu kuhusu mwenzake lakini sio vyake, atataka yako simu ajue ni nani anapiga au kutuma sms, atataka kujua unaongea na nani na kwanini.Hii sio dalili ya mahusiano mazuri.

kujipendelea (self-centeredness)

Hakuna maana ya mapenzi kama mwenzi wako anakuwa akijali nafsi yake kuliko yako, maana ya mapenzi ni kujitoa muhanga kwa kila kitu , mapenzi mazuri ni yale ambayo kila upande unakuwa ukifaidi kile mlicholenga kukianzisha , lakini kama mmoja ananungunika na mwingine anafurahia na kuona sawa tu basi hayo sio mapenzi, ONDOKA HARAKA.

Kutaka kujimilikisha

Hatukatai kuhusu kumpenda mtu mpaka kumuonea wivu, lakini kuna ule wivu tunasema ni ujinga, wivu ambao anataka kujimilikisha wewe kuwa ndio wake kwa kila kitu.Wivu ambao kila sehemu na kila kitu chako basi ni lazima kipitie kwake, hii inachosha na kumfanya mmoja wenu akose amani ya maisha na mapenzi pia.

Ukosefu endelevu.

Kuna mtu anaweza kuwa amekuchoka lakini hataki tu kusema kwa sababu hataki kuwa sababu ,mtu huyu anaweza kuwa ni mwenye vituko na makosa ya kila siku yanayojirudia kila mara na kukufanya kuchoka.Fikiria kwamba amekuwa kila siku akifanya kosa moja ambalo kwa namna moja ama nyingine ameshajua kuwa linakukwaza , lakini cha ajabu kwa sababu ya mapenzi akiomba msamaha Unakuwa laini, Amka na anza kuchukua hatua hapo.

Udanganyifu uliopitiliza.

Ujawahi kusikia kesi ya kuwa mtu anakuwa akifanya kitu sio kwa sababu akili yake inataka afanye kitu fulani, lakini kwa sababu ya ushawishi kutoka kwa mtu anaempenda anajikuta anaweza kufanya chochote tu , hii utokea sana katika mahusiano ya sasa, mmoja wenu anakuwa na maneno ya kukulaghai na kukufanya ukubaliane na kile anataka yeye wakati mwisho wa siku kitawaingiza katika matatizo tena hasa kwa upande wako.

NB;-Hakuna mtu asiependa amani kwa kila kitu, kuwa kwenye mahusiano au kuwa na mtu unaempenda kusikufanye ukaona kuwa maisha hayana maana kabisa, unachopaswa kujua ni kwamba , pale unapoamua kuwa katika mahusiano kitu kikubwa cha kuzingatia ni amani ya moyo wako , hivyo tafuta mahusiano yenye afya sio kupelekwa tu kwa sababu unahitaji mahusiano.
Share:

Mambo 5 Ya Kufanya Ili Mpenzi Wako Azidi Kukupenda


Mapenzi ni kitendawili lakini ukiyapatia yanaweza kuwa matamu sana. Lakini mapenzi yanahitaji kazi unahitaji kujitahidi kuyajenga kila siku ili yasiyumbe wala kubomoka hasa ukiwa kwenye ndoa au mahusiano.

Mkiwa wawili kwenye mahusiano kwa muda mrefu suala la kuchokana lipo na ni muhimu sana kuhakikisha jambo kama hili halitokei kwenye mahusiano yako kwani mkishaanza kuchokana ndio utakuwa mwisho wenu.



Leo tutaangalia mbinu mbali mbali zitakazokusaidia kuhakikisha kuwa mapenzi yenu hayachuji na njia utakazotumia kuhakikisha unakoleza mapenzi ili yazidi kuwaka na kuchanua.

Ili Mahusiano yoyote yadumu ni unahitaji kuyafanyia kazi na uvumilivu ni muhimu sana zifuatazo ni njia na mambo muhimu ya kufanya ili mpenzi wako azidi kukupenda;

1. Kujiamini ni muhimu

Hakuna kitu kinachomvutia mwanaume yoyote kama mwanamke ambaye anajiamini na imara, yaani mwanamke ukianza kujiamini na uzuri wako na imani yako basi mwanaume atazidi kuvutiwa na ujasiri wako na akili yako.

2. Kuwa msikivu na mwenye huruma

Ili kumuelewa mpenzi wako inabidi uwe msikivu, kumsikiliza mtu ndio njia pekee ya kumwelewa. Usikimbilie kumkosoa pale tatizo linapotokea kwa kufanya hivi utaweza kumwonyesha kuwa wewe sio tu mpenzi wake bali rafiki pia.

3. Mthamini Mpenzi wako

Kwenye mapenzi ni lazima kila mmoja amthamini mwenzie kwa njia hii utamuonyesha kuwa unatambua mchango wake kwenye maisha yako na kitu kingine usije ukajaribu kumbadili mpenzi wako ili awe utakavyo wewe bali mthamini kwa vile alivyo kwani ndivyo ulivyompenda.

4. Jifunze vitu vipya kila siku

Ili mapenzi yenu yasichuje basi lazima yaende na wakati ni muhimu kubadilika ili kuwe na hamu fulani mabadiliko haya yanaweza kuwa katika mambo yenu ya chumbani au hata vitu vya kufanya kama kuangalia movie labda au hata kusafiri sehemu mpya.

5. Kuwa mpenzi bora lakini zaidi rafiki wa kweli

Wapenzi ambao wana uhusiano mzuri ni wale ambao pia wana ukaribu wa kirafiki ili wewe na mpenzi wako muweze kudumu zaidi na kupendana ni lazima muwe marafiki hii itawasaidia kuwa karibu zaidi na kuwa wawazi kwa chochote kitakachotokea.
Share:

SMS Za kumsihi mpenzi wako asikuache

Image result for SMS ya kumsihi mpenzi wako asikuacheT.gifSMS nzuri ya salamu kwa mpenzi wako

Furaha ni kawaida yangu, kununa si busara kwangu, kuishi
nawewe vizuri ni sehemu ya Maisha yangu,
kukusalimia ni hulka ya Moyo wangu, Uhali gani mpenzi

πŸ”₯♥♥♥


T.gifMeseji nzuri ya kimahaba ya salamu kwa mpenzi

Pokea sms yangu iliyojaa utamu, nimeipamba kwa maneno
laini yenye ladha adimu, utamu wake ni kama
apple haufanani na ndimu, nimeituma kwako sms hii ikuletee
salamu "UHALI GANI MPENZI?"

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS ya kumtumia mpenzi wako kumwambia kuwa unamjali na kumpenda milele

Tambua kuwa nakujali
Furahia kwamba nitakuwa na wewe
Katika siku zote za maisha yangu
Nitakupenda bila kikomo milele

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS ya kumsihi mpenzi wako asiende kwa mwingine

Nakupenda sana mwandani wangu ndiyo maana moyo wangu
hupatwa kidonda ninaokuona na mwingine hasa anapokuwa hana
sifa, nahisi kama anakutumia wewe kama mdori wake wa
kumfurahisha. Uwe makini ua la moyo wangu.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS ya kumsisitiza mpenzi wako asiende kwa mwingine

chekecho la huba ,toka uvunguni mwa moyo wangu
navika moyo wako taji la upendo,na kupulizia marashi ya hubaa ,usimpe mwingine mi ndiye ninayejua kulea.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS nzuri ya kumtumia mpenzi wako mpya

Mpenzi wangu T tambua kuwa ulimwengu tunaoishi una mambo
muhimu matatu. Jambo la kwanza ni kumpata umpendaye, la
pili ni kupata atakayekupenda la tatu ambalo ni kubwa
kuliko yote ni kwa jambo la kwanza na la pili kuungana
pamoja.
Nashukuru nimekupata wewe nikupendaye, naomba unipende na uungane nami

πŸ”₯♥♥♥


T.gifMeseji ya kumwambia mpenzi wako asiwaze hata siku moja kuwa unawea kumuacha

Asali wa moyo wangu, fahamu kuwa unaweza kuamini kwamba
mwanga wa nyota unaweza kuunguza nyumba, jua linaweza
kusimama, lakini usiwaze hata siku moja kuwa naweza
kukuacha.

πŸ”₯♥♥♥


T.gifSMS ya kumsihi mpenzi wako asikuache

Uchungu wa kifo hauna tofauti na maumivu nitakayoyapata ukiniachana, mpenzi usiniache nami siko tayari kukuacha.

πŸ”₯♥♥♥

Share:

hatua ya kuamua kuelekea marafiki wapya


Maisha ya kisasa ni ya kuchemsha, yenye kupumua na haikuruhusu kuacha. Hii ndio wakati wa teknolojia ya kisasa, kasi ya haraka na habari za haraka za umeme. Tunakula chakula cha haraka, tunauvaa nguo kwa mtindo wa haraka na kujifunza msaada wa kasi ya dating. Maana ya tukio hilo ni ziara ya haraka, kuweka "ukanda wa conveyor".


Speeddating ni kupata umaarufu, wengi wanataka kujaribu aina hii ya burudani na wako tayari kulipa. Usajili katika chama hupanda kutoka rubles 1.5 hadi 5,000, kunywa na chakula kwa gharama yako, hivyo kazi hii si ya bei nafuu. Waandaaji hujaribu kuunda hali nzuri zaidi kwenye tukio hilo. Hata kama hupendi mtu yeyote, utatumia jioni isiyo nahau katika mgahawa mzuri au katika cafe yenye hali nzuri.

Bila shaka, wasichana wengine wanaweza kufikiri kwamba tayari wameishi kwenye hatua kama hiyo ya upweke ambao tayari wako tayari kutoa pesa ili ujue na wavulana. Lakini usiache kusudi lako - unaweza kutafuta furaha kila mahali na kila mahali, na hakuna mtu anayepaswa kulaumu kwa hili. Kupumzika, kufurahia utaratibu wa dating na ufumbuzi. Na, mwishoni, angalau kulipa uwekezaji kwa ukamilifu.

Sio ukweli kwamba utapata upendo wako kwenye tarehe hizo na kuolewa haraka, lakini unaweza tu kufanya marafiki muhimu, kukutana na watu unaowapenda tena, na huenda kuna tena. Matokeo ya speeddating si ya kipekee na mabadiliko yoyote ya matukio yanawezekana. Labda tarehe ya mini, ambayo hupendi, hatimaye kukua kuwa upendo wa kweli.

Vidokezo vichache kwa wale walioamua juu ya burudani hizo


Kwanza, ni vyema mara moja kutafakari kwenye wimbi jema na hamu ya kukutana au angalau kuwa na jioni nzuri. Kima cha chini - unaweza kufanya marafiki wapya na viungo muhimu, na upeo - kukutana na mtu ambaye atakuwa mpenzi wako, na baadaye mume.



Pili, kwenda kwenye tukio peke yake, bila marafiki na wa kike, kwa hiyo kuna nafasi kubwa ya kupata ujuzi, kwa sababu huna mtu wa kujadili wanaume kati ya marafiki. Wakati mwingine, majadiliano kama hayo yanaweza kusababisha kuwaangamiza waheshimiwa wenye uwezo ambao wanataka kukutana nawe. Na, kwa hakika, inawezekana kwamba utampenda kijana huyo, na hutaki kumshirikisha.



Dakika tano kuamua kila kitu


Katika dakika tano unahitaji kujionyesha kwa ufanisi iwezekanavyo, hivyo uandae. Fikiria mapema kwamba unaweza kuzungumza juu yako mwenyewe, juu ya vitendo vyako, mawazo, kitu ambacho kitakuweka mbali na umati na nini unakumbuka kwa wanaume. Jaribu kupata ardhi ya kawaida na mtu unayemjua. Lakini kumbuka kuwa hii sio mahojiano, na uwasilishaji wa ukweli wa biografia yako hauwezekani kukamata mtu. Lakini pia kimya kimya pia sio thamani - chagua maana ya dhahabu na usahau kusikiliza mpinzani wako. Wanaume wengi ni ndogo sana na huuliza maswali. Lakini msiwe na tamaa kwa mtu huyo mara moja, kumpa nafasi, kwa sababu ana wasiwasi. Si rahisi kumvutia mara moja wasichana kadhaa, kuna watu ambao wanaona kuwa vigumu kufahamu moja. Lakini hiyo haina maana kwamba yeye si kama hiyo.



Smile, kwa jambo la kwanza unalenga ni tabasamu yako wazi. Fanya tabasamu yako ishara, inayoonyesha. Kusahau kuhusu shida na matatizo uliyo nayo. Kuwa hapa na sasa, na jaribu kuwa wewe mwenyewe na kujitegemea. Kusikiliza msemaji wako na utafanikiwa.



Makampuni ya kuandaa vyama vidogo, ni bora kuangalia kwenye mtandao, wakati huo huo kusoma wasifu wa watu ambao tayari wamejaribu burudani kwao wenyewe. Usiogope kwamba waandaaji watakuomba uingie mahojiano mafupi. Maswali juu ya mapato hayataulizwa kwako, tu akaunti ya kina ya wewe mwenyewe, maslahi, kazi, vitendo, kazi. Uchaguzi wa makini wa washiriki umefanyika ili kupata watu wanaofaa, kutoa hatua za usalama, ili uwe na fursa zote za kukutana na mtu anayestahili na mwenye kuvutia, sio mvulana kutoka kwenye lango.
Share:

Jinsi ya kujishughulisha na uhusiano mpya wa upendo

Related image

Uhusiano kati ya wanaume na wanawake huanza na urafiki. Usijijikeze, kwamba katika uhusiano wa kimapenzi kila kitu kitakuwa njia yako. Usiache juu ya marafiki wapya tu kwa sababu ulifikiwa mahali tofauti na haukufikiri kuwa ni heshima. Usiogope kutokuwa na uhakika au kinyume chake. Ujuzi na mtu ambaye anakupendeza ni nzuri zaidi kuliko kiti cha nyumba moja, na wivu marafiki wenye mafanikio.


Wanaume wenye heshima wanajue msichana kuwa rafiki na mmoja wake, na kisha kuoa na kuunda familia yenye nguvu, yenye furaha. Wanaume hao kwa heshima na kwa usahihi kumtendea mwanamke si tu wakati wa urafiki, bali maisha yao yote. Wasichana waaminifu kudumisha uhusiano wa upendo na mtu mmoja tu na daima kujaribu kujenga familia pamoja naye. Leo tutazungumzia kuhusu jinsi ya kujijiunga na uhusiano mpya wa upendo. "

Kuna sababu nyingi ambazo watu hufanya uhusiano wa karibu na wenye upendo. Mtu yeyote ana ndoto ya ukaribu kwamba uhusiano wa roho hutoa. Tunapoanguka katika upendo, tunahisi jinsi maisha yanapaswa kuwa kama na yale tuliyesuzuia. Hata baada ya kupata tamaa nyingi katika upendo, tunaendelea kutafuta upendo wa kweli. Hakuna mtu anayeweza kuondokana na hamu ya kupoteza na upendo wa kweli.

Lakini kwa sababu fulani, kila wakati tunapokuja kwa upendo, kuna baadhi ya sababu zinazozuia sisi kupata hisia halisi. Baada ya kubadili washirika kadhaa, tunaona kuwa uhusiano wowote mpya unakaribia kwa kasi. Kwa kila upendo mpya, "asubuhi" inakuwa mfupi na mfupi. Matokeo yake, kwa ujumla, yatatoweka na kwa ndoto yake ili kupata upendo wa kweli, unaweza kusema faida milele. Tunapoanguka kwa upendo, tunakuwa hatari sana. Baada ya kupima tamaa katika upendo, tunaamua kujijulisha kwa kiwango hicho.

Ikiwa tunajiangalia wenyewe kutoka nje, tutaona kwamba katika uhusiano wote usiofanikiwa tuna hatia. Baada ya kuanguka kwa upendo na mtu mwingine, tunakabiliwa na hofu na kujidharau wenyewe. Tunahitaji kutambua na kufuatilia maonyesho haya katika nafsi yetu. Ikiwa hatupendi sisi wenyewe, hakuna mtu atakayependa. Tunapojidharau wenyewe, tunadhani kwamba wengine pia wanatuangalia. Ili kuepuka upendo usio na furaha, unapaswa kufanya kazi mwenyewe, juu ya hofu yako na dharau kwako mwenyewe.

Ikiwa tunajua na kujitengeneza wenyewe, itatusaidia kuboresha uhusiano wetu wa kibinafsi. Kwa ujumla, tunawatendea watu jinsi tunavyojitendea. Ikiwa mtu ni katika upendo mwenye furaha, basi anajua jinsi ya kujipenda mwenyewe. Ndoa yenye furaha ina maana kwamba sisi ni haki kabisa juu yetu wenyewe.

Mara nyingi mara nyingi wanapendeza sana kutafuta mpenzi mzuri na kusahau kuhusu sheria za mahusiano ya kibinafsi. Sheria hii ni kwamba mpenzi ni kitu lakini kioo sisi wenyewe. Watu wanajaribu kuelewa kama mpenzi wao anapenda au hawapendi na kusahau juu ya nguvu zao juu ya uhusiano, kusahau kwamba kila kitu ni mikononi mwao.

Mtu yeyote anachagua mahusiano ya upendo kwa njia kamili kabisa na ya kuchagua. Mara nyingi mpenzi tunayeacha katika maisha yetu ana tabia sawa na yako. Lakini hatujui au hatutaki kuona jambo hili. Na wakati mpenzi atakayekasirika na sifa zake za tabia, hatupaswi kusahau kuwa hizi ni tabia yako ya tabia ambayo hutaki kuiona.

Tunachagua wale washirika ambao wanaweza kukufanya uwe na furaha zaidi na sasa. Chukua kioo na ujiangalia. Kioo kitatusaidia kujua ambao sisi ni nani na nini tunahitaji kujifunza. Tunawavutia watu ambao wanaonyesha hisia zetu, mawazo na vitendo. Ili kuona katika mpendwa, ni ubora mzuri, na kisha kutambua kwamba ubora huu umekuwepo, hutoa furaha kubwa.

Mara nyingi hutokea kwamba unakumbwa na mtu mwingine na sifa zinazohusiana na yako. Lakini baada ya kile ulichovutia sana, huanza kuvuta. Watu tofauti kabisa hawawezi kuishi pamoja ikiwa hawapati mfululizo wa maslahi yao. Kwa bora, wataishi sawa na kila mmoja, wakiongea daima, ambao maisha yao ni bora zaidi. Mahusiano hayaruhusu tu kutambua mtu mwingine, bali pia kutupa kuelewa matatizo yetu binafsi na maumivu ya akili. Na hapa uhusiano hutusaidia kuponywa katika shida zetu za zamani.

Kutafuta kutoka kwa mpenzi kila kitu unachotaka, unatumia uwezo wa ushirikiano. Hii ni muhimu hasa katika ndoa. Ikiwa kitu haipatani na uhusiano wako, fanya nguvu zako. Ikiwa ungependa ndoa ya uhusiano mzuri, hakuna mtu anayeweza kukuzuia kufanya hivyo. Ili kufanya hivyo, unahitaji kukusanya nguvu zako zote na kuielekeza kwa njia sahihi.

Wengi hawataki kujua kuhusu wao wenyewe ukweli na kuishi katika ulimwengu wao uliotengenezwa. Katika ulimwengu ambapo matukio mazuri na sio sana yanaanguka juu ya vichwa vyetu. Ambapo tumebarikiwa au kinyume chake ni laana na hawezi kufanya chochote kwa furaha yetu. Lakini yote haya ni udanganyifu tu. Kwa kweli, tunajenga hatima yetu wenyewe, na tunaweza tu kujihukumu wenyewe kwa maafa yetu. Na pia kwa wakati wa furaha tunapaswa tu kujiunga wenyewe. Huu ni elixir ya uchawi, ambayo itafungua kabla ya ulimwengu wa fursa mpya.

Ikiwa wewe ni peke yake na umeamua kuanzisha uhusiano mpya, fikiria na kufikiri jinsi unavyofikiria mpenzi wako wa baadaye. Inaweza kuwa ngumu kuamini, lakini utamvutia mtu ambaye uliota ndoto. Kuanzisha mpenzi wako wa baadaye, mawazo yako lazima yawe sahihi na maalum. Usisahau kwamba tunaunda ulimwengu unaozunguka na mawazo yetu. Yote iliyokutokea katika maisha ilikuwa katika mawazo yako au tamaa. Kwa hiyo fanya faida ya hali hii na kujenga mwenyewe maisha unayoota, fikiria tu ya mema.

Kipengele muhimu cha mahusiano, na hasa wa karibu, ni mawasiliano. Usiogope kuonyesha hisia kwa mpenzi wako. Ikiwa haujui hisia zako, una nafasi chache za uhusiano na mpenzi. Lakini usivunja moyo, kila mtu anaweza kujifunza kufahamu hisia zao. Hii inahitaji tu mazoezi na uamuzi. Jaribu kufungua roho yako yote kwa mpenzi wako. Ikiwa yeye hajakuelewa na anaamua kugawanya, inamaanisha kwamba hutambatana. Utakutana na mpenzi mwingine, ikiwa bila shaka utakuwa na fursa na uwe mwenyewe. Sasa unajua jinsi ya kujiweka kwa uhusiano mpya wa upendo.
Share:

Hiki ni kitu muhimu kwa kila mwanamke kukizingatia



WENGI kati ya wasichana walio katika ndoa ama mahusiano ya muda mrefu ni wepesi sana kujihusisha na vitendo vya usaliti. Hii ni tafiti rasmi. Ni tafiti inayokera na kuumiza ila huo ndiyo ukweli.

Siku kadhaa nyuma niliwahi kulijadili hili suala katika namna ya kuwaasa wanaume kuwa makini na kuacha kuishi kimazoea na wake zao ili kupambana na changamoto hii. Leo nataka tujadili hili suala katika mtindo tofauti kidogo. Leo nataka kuongea zaidi na wanawake.

Japo mwanamke na mwanaume ni binadamu ambao wote hukumbwa na tamaa za kimwili na kuwa na hisia za upendo ila ukweli ulio dhahiri ni kwamba, tamaduni na mazingira ya kidunia yamewapa zaidi mamlaka wanaume kuwaeleza wanawake namna wanavyojisikia juu yao na wanawake wao kubaki na jukumu ama la kukubali ama kukataa matakwa ya wanaume husika.

Kitu hiki kinaweza kutafsiriwa kuwa kimemuweka mwanamke katika kundi la muwindwa huku mwanaume akijiweka katika kundi la muwindaji. Hali hii ndiyo imesababisha wanawake wakumbwe na changamoto zaidi ya kutongozwa (kuhitajiwa na wanaume kwa ajili ya mapenzi) kuliko wanaume.

Kutokana na mwanamke kuwa katika kundi la muwindwa, mara nyingi hujikuta akikutana na wawindaji (wanaume) wakiwa na mbinu na mikakati mbali mbali kwa ajili ya kuwa naye.

Kwa baadhi ya wanawake hali hii huitafsiri kuwa ni kutokana na uzuri wao ama wana bahati sana katika maisha. Kitu ambacho wengi wanashindwa kutambua ni kwamba wakati mwingine wanaume hutongoza hata bila sababu ila hujikuta tu wakitongoza wanawake kwa sababu anaona akiacha kutongoza uanaume wake utashindwa kutafsirika vema.

Wanawake wengi walio katika mahusiano kwa muda mrefu wamejikuta ni watu rahisi sana kuingia katika mitego ya wanaume wanaowatongoza kwa sababu ya kudhani huko nje kuna mambo mengi mazuri, ya kuleta furaha na amani kuliko ndani ya mahusiano yao.

Hii inatokana na ukweli kwamba, wawindaji hao (wanaume) huja na maneno mazuri na ahadi kemkem zinazopunguza ufahamu wa wanawake husika na kuwaona wawindaji hao ndio hasa watu walio wahitaji katika maisha yao.

Wakati wakiwaza haya, wanawake hawa huwa wanasahau kuwa, upya wao kwa wanaume husika pamoja na wao kuwa katika ndoa ama mahusiano na wanaume wengine ndiyo hasa huwa chanzo cha wao kubabaikiwa.

Hii inatokana na ukweli kwamba, wanawake walio katika ndoa huwa siyo wasumbufu sana kama wanawake wengine wasio katika ndoa.

Tafiti zinajuza, kwa sababu nia ya wanaume wengi wenye kuwatongoza wau walio katika mahusiano huwa ni tamaa za mwili za muda mfupi, hufurahia maisha na wanawake hawa kwa sababu huwa hawaulizii ulizii sana suala la kutaka kuolewa.

Pia uzuri wa wanawake hawa walio katika ndoa ama mahusiano ya muda mrefu huwa na shida na vitu vidogo vidogo tu kwa sababu majukumu yote ya msingi huwa yanamalizwa na waume zao.

Wakati fikra za wanaume hawa wanaotoka na wanawake walio katika ndoa huwa ni mahusiano ya muda mfupi ila ukweli ni kwamba wanawake wenyewe huwa wanajikuta wakitopea sana kwa hawa wanaume na kujikuta wakianza visa na dharau kwa wanaume zao kwa kuona kama wameishiwa ama watu wasio wa kisasa sana.

Matokeo yake hujikuta wakisababisha migogoro mikubwa katika ndoa zao ambayo ama italegeza thamani na hadhi ya mahusiano yao au kuvunja kabisa ndoa zao kitu kinachowapelekea baadaye kujikuta katika majuto makuu.

Ni vema wanawake wakatambua ni rahisi sana kwa aliye ndani ya nyumba kutamani kutoka nje ila jua thamani na hdhi ya binadamu hupatikana akiwa anaishi ndani na siyo nje kama miti ama matunda.
Share:

Zifahamu njia za kudumisha uhusiano wako


Mahusiano ya mapenzi yamekuwa moja ya jambo linalolalamikiwa sana na vijana wengi huku wengi wakisema katika dunia ya sasa hakuna mapenzi ya kweli huku wengine wakisema usaliti na kuumizana kumekuwa na nafasi kubwa zaidi kuliko wale ambao


wanakuwa na mipango ya dhati na mambo mbalimbali yametajwa kuchangia usaliti ikiwemo tamaa ya pesa na maisha mazuri kwa mabinti, na tamaa ya ngono kwa baadhi ya wanaume.

Kupitia kipindi cha Late Night kinachorushwa East Africa Radio jana walikuwa wakielezea namna ambavyo mtu mmoja mmoja anaweza kushiriki kudumisha uhusiano wake na mpenzi wake katika kufikia malengo ya kuwa kitu kimoja kama mume na mke, na haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki kutoka katika ukurasa wa facebook wa East Afrca Radio www.facebook.com/EARadio wakionyesha ni jinsi gani wao wanashiriki katika kudumisha upendo na kuepusha kusalitiwa na kuachwa kama si kuumizwa moyo.

West Lif Ema Anger: "Kwanza inapaswa umsome mpenzi wako anataka nini na anataka wewe uweje bila kusahau uaminifu na upendo wa kweli kati yenu ili muweze kusihi kwa amani na upendo siku zote"

Hope Chopa Hope Chopa: "Kupendana ,kujaliana ,kusameheana na kusikiliza hisia za mwenzako lakini pia uvumilivu wa hali ya juu na uwazi. Ila cha muhimu ni kumpenda anayekupenda kweli na si yule anayependa kitu kwa maana kikiisha au kisipo kuwepo mapenz hugeuka kero ndani au kati yenu na kupelekea amani na furaha kutoweka kabisaa kwani hali hiyo itapelekea kuacha au kusaliti penzi lenu na mwisho wa siku mkajikuta matatizoni"

Kidoti Tillya: "Ili kudumisha mahusiano ni upendo wa dhati kwa kila mmoja, pili kila mmoja kujalii hisia za mwenzake yakizingatiwa hayo mahusiano lazima yawe strong."

Irinda Marwa: "Nazungumza nae sana haijalishi limetokea tatizo gani tunakaa pamoja, tunaongea tunasikilizana maisha yanaendelea.....Huwa tunazungumza kwa uwazi kabisa kama mtu na rafiki yake na unashangaa hata kama tulikuwa na tatizo kubwa linaisha tukiwa na furaha na amani inarudi kati yetu."
Share:

Maneno 4 Rahisi Lakini Muhimu Ambayo Mke Anahitaji Kusikia Kila Siku





Mawasiliano mazuri kati ya mke na mme ni muhimu sana kwa ajili ya ustawi wa mahusiano ya wawili wapendanao. Inasemwa kuwa kuvunjika kwa mawasilioano pekee katika mahusiano kunasababisha mifarakano au kuvunjika kwa mahusaiano kati ya mke na mme kuliko sababu nyingine.

Wataalamu wa mapenzi na hisia za binadamu wanaeleza kuwa wanawake wanaguswa sana kwa maneno kuliko vitendo. Sauti na maneno mazuri ni vitu ambvyo vinawafanya wawe katika wakati mzuri sana kihisia. Wanaume wao wamefahamika kuwa wanavutwa zaidi kwa kuona kuliko kusikia.

Kwa msingi huu basi ni muhimusana kwa wanaume walio katika mahusiano ya mapenzi kufahamu siri hii juu ya wenza wao wanawake. Ukitaka kuifanya siku ya mpenzi wako nzuri basi zingatia maneno yako na sauti yako iwe katika kiwango kinachofaa.

Yafuatayo ni maneno manne muhimu kuyasema kila siku kwa mkeo na yataleta mabadiliko makubwa katika mahusiano yenu. Maneno haya yanalainisha moyo,yanajenga uaminifu,yanazidisha upendo,yanaponya majeraha ya mapenzi na yanaleta furaha kati ya wapenzi:
Neno #1. “Wewe Ni Mwanamke Mzuri”



Inawezekana uzuri ni sababu mojawapo ya kumuoa au kuwa naye. Basi hakikisha unamkumbusha kila mara. Wanawake wanahitaji sana kuhakikishiwa kuwa ni wazuri na wanavutia. Ni hatari sana kama hufanyi hivi kwa mkeo,nakuhakikishia wanahitaji kusikia maneno haya. Usipomwambia kuna mtu atamwambia barabarani au kazini na hii ni hatari.

Wanawake wasio ambiwa mara kwa mara kuwa ni wazuri huhangaika sana juu ya kubadilisha mavazi yao na vipodozi. Ikibidi wanaweza wakafikia kuvaa mavazi yasiyo na heshima sana kwa mtazamo wa jamii anayoishi. Hii ni katika kutafuta mrejesho kuwa ni mzuri.

Kama anatumia sana vipodozi na wewe hupendi basi mwambie ni mzuri hasa akiwa asilia,hivyo hahitaji vipodozi vingi.
Neno #2. “Umependeza”



Hili linaendana na la kwanza hapo juu lakini kupendeza sio lazima uwe mzuri. Uzuri unaweza ukawa wa sura,umbo au tabia zake. Kupendeza ni kutokana na mapambo na mavazi ambayo mtu anavaa.

Kama kuna mambo makubwa ambayo yanawachukulia muda mwingi wanawake wengi basi ni urembo hasa wa mavazi,nywele na vipodozi. Wafanya biashara wajanja wanaweka nguvu zao eneo hili – kutoa huduma za wanawake.

Wanawake wanahitaji sana kuonekana wamependeza hasa toka kwa wapenzi wao. Mrejesho huu ni muhimu kwao na kunawafanya wajisikie vizuri ,kujiamini na kujiona wa thamani. Mwambie mkeo kila siku asubuhi akitoka nyumbani au kila mnapotoka pamoja. Mwambie kila akibadilisha aina ya ususi wa nywele zake.
Neno #3: “Asante”



Kwa kweli mke ndiye mtendaji wa mambo mengi nyumbani. Hata kama kuna wasaidizi bado kunahitaji uongozi na bila shaka mke ni kiongozi wa yote haya nyumbani kwa walio wengi.

Utakuta nguo ni safi,chakula ki tayari,watoto wameoshwa na kuvalishwa na mengine mengi. Kuna kila sababu ya kusema “asante”.

Asante ina maajabu makubwa kama ikitolewa kwa jinsi inavyostahili na kwa dhati. Kwanza humfanya anayeambiwa ajione wa thamani sana kwako. Pili humfanya anayefanya aongeze bidii kwa yale anayoyafanya.

Hivyo usiache kushukuru kila siku kwa yale mkeo anayoyafanya. Kunawezekana mengine yakawa si mazuri,lakini hakutakosekana zuri la kushukuru.

Mwambie “Asante Mpenzi” , “Asante Mke Wangu” na maisha yenu yatakuwa mazuri na yenye furaha.

Fanya kwa vitendo pia,mfano nunua hata kitenge tu na umshangaze kwa zawadi. Mwambie “asante kwa kuwa mama mzuri wa watoto wetu” au “Asante kwa kuwa mke mzuri na rafiki mzuri kwangu”.
Neno #4: “Nakupenda”



Kupendwa ni mojawapo ya vitu ambavyo binadamu anahitaji sana. Chukulia mtoto mfano,toka tukiwa watoto kupendwa ni kitu kinachohitajika sana na kinapokosekana kuna madhara makubwa yanayotokea ikiwemo mtoto kutojipenda mwenyewe na kutojiona wa thamani. Kwa wanawake halikadharika,japo ni wakubwa tayari lakini kasumba ya utotoni imo bado ndani yetu na mahitaji ni yaleyale.

Ukiangalia vizuri mahangaiko yote ya mwanamke juu ya urembo na mavazi utaona kuwa ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Au kujinyima na kuishi katika mwenendo ambao wewe kama mume unafikiri ni vizuri au jamii inafikiri ni vizuri ni kutaka kuhakikisha kuwa anapendwa. Basi kwa kumtamkia kuwa unampenda mara nyingi kadili utakavyoweza inampa kujiamini kwa jinsi alivyo na kwa yale anayoyafanya.

Kumwambia mkeo kuwa unampenda na kuonyesha kwa matendo kunamfanya naye akupende zaidi.

Neno hili likitumika kwa dhati na sio kusema tu lina maajabu makubwa katika kuboresha mahusiano ya wenza wapendanao.
Fanya kwa Dhati na Upendo

Maneno haya manne yana maajabu makubwa kama yakitekelezwa ipasavyo. Kwanza ni muhimu sana ukayasema kwa dhati na kumaanisha toka moyoni. Kunaweza kukawa na mambo yasiyofikia viwango vya kushukuru au kusifia lakini uanaweza ukaanza na yale machache yaliyopo. Baadae utagundua kuwa hata mengine yanarekebishwa na kufanywa kwa uzuri.

Maajabu ya maneno haya ni katika kubadilisha moyo wa mke na tabia na matendo yake. Ukiyatumia kwa kiasi kinachofaa na kwa kuyamaanisha utafanikiwa na utaboresha mahusianao yenu.

Kama una mawazo ya kuchangia mada hii tuandikie katika kisanduku cha majibu hapa chini.
Share:

Njia 5 za Kudumisha Mahusiano ya Mapenzi


Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.”

Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi.

Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea,yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia. Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana
Uaminifu

Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote.

Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako.

Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano.

Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli mara zote. Ongeeni juu ya mipango na mawazo yenu bila kufichana.

Watambulishe kwa mpenzi wako ndugu ,jamaa na marafiki wakaribu ili kumpa mwenza wako amani.


Weka muda kwajili ya Mwenza wako

Mahusiano mazuri kati ya wapenzi yanahitaji muda wa wapenzi hao kukaa pamoja. Wapenzi wasio na muda wa kukaa wana hatari ya kupoteza mvuto wa mahusiano yao na hivyo kuhatarisha uhai wa mapenzi kati yao.

Kama wapenzi wapo mbali mbali basi wanahitaji kuweka muda wa kuongea kila inapowezekana.

Tafuta muda wa kutoka pamoja,hata kama mtaenda mkahawani kunywa chai au juisi tu,inatosha sana na inawaweka karibu zaidi.
Mawasiliano

Mawasiliano ni muhimu sana baina ya wapenzi.

Hata kama umebanwa na kazi pata dakika chache za kuongea na mpezi wako na kumtaka hali. Andika hata ujumbe wa maneno au barua pepe. Mwambie mpenzi wako ulipo kila mara inapobidi ili kumjengea imani na wewe na kumpa amani moyoni. Tuma ramani ya mahali ulipo kama unatumia simu ya “Smart” (Tuma location kwenye whatsapp)

Mawasiliano ni ufunguo wa kudumisha upendo.

Wakati kuwasiliana na mpendwa wako, kumbuka kwamba upendo ni muhimu. Ongea toka moyoni na si kwa ajili ya kutimiza wajibu tu,kwani mpezi wako atajua tu kama hakuna mahaba katika mawasiliano yenu hivyo kutoleta faida ile inayotegemewa.

Mawasiliano mengine ni yale ya kuelezana yaliyo moyoni. Mweleze mwenza wako linalokusibu ili kupata ufumbuzi wa pamoja. Wapenzi wanaoongea kwa utulivu siku zote watakuwa pamoja.
Zawadi

Tafuta kitu cha kumpa mpenzi wako. Si lazima kiwe na thamani kubwa.Inaweza ikawa pipi au matunda tu.

Mnunulie zawadi kila inapowezekana hasa unaposafiri au katika siku yake ya kuzaliwa.
Onyesha Upendo Wako

Kila mtu anajinsi yake tofauti ya kuonyesha upendo, lakini vyovyote itavyokuwa ni jambo la muhimu sana kuonyesha hisia zako kwa mpenzi wako.

Mara nyingi wapenzi wa muda mrefu wanasahau juu ya hili.

Maneno kama “Nakupenda”au majina ya mahaba kama “Mpenzi” au ”La-azizi” yanachangia sana kuonyesha mapenzi na kumfanya mwenza wako kujisikia vizuri.

Maneno haya yanaposemwa kwa hisia halisi na toka moyoni yana mchango mkubwa katika kuboresha mahusiano.
Share:

Faida tano (5) za kuoa au kuolewa na mtu sahihi




Je unajua kuwa swala la ndoa lina nafasi kubwa sana katika swala la wewe kuishi ndoto zako? Ukifanya uamuzi mzuri katika swala la ndoa utapa mwenzi ambaye hatokuwa mzigo na kikwazo kwako katika kuishi ndoto zako.

Zifutazo ndizo faida za kuoa au kuolewa na mtu sahihi.



Atakujali na kukutia moyo kila wakati.
Mtapanga mipango mbali mbali ya maendeleo pamoja.
Mtasaidiana na kutiana moyo wakati wa shida.
Mtahamasishana ili kuhakikisha mnafikia ndoto zenu.
Atakusaidia kutimiza majukumu na mipango mbalimbali.



Ikiwa basi hukupata mtu stahiki katika ndoa, faida hizo hapo juu zitakuwa kinyume chake na mtokeo yake utakosa furaha na kuishi masha ya mahangaiko ambayo katu hutofikia ndoto zako.
Share:

Mambo muhimu mnayopaswa kufanya ili kuyafurahia mahusiano yenu



Mahusiano ya mwanaume na mwanamke hukutanisha watu kutoka koo mbalimbali. Kila mtu anakuwa amelelewa tofauti kwa wazazi wake. Tabia haziwezi kufanana. Huyu anaweza kuwa na tabia fulani ambayo mwenzake anakuwa hana. Mnapokutana wawili, ili muweze kwenda sawa ni lazima muelewane tabia, mshibane na kila mmoja amvumilie mwenzake. Hakuna binadamu aliyekamilika. Inawezekana kuna vitu ambavyo mwenzako anavyo, na pengine si vizuri. Suala la msingi ni kupata muda sahihi wa kumbadilisha mwenzako ili naye aweze kukubaliana na mabadiliko unayotaka kumpa, na mwisho wa siku mtakwenda sawa.

Unapomuelekeza mwenzako juu ya tabia fulani, unapaswa kutumia lugha rafiki; lugha ya mtu na mpenzi wake! Ambayo itamfanya asijisikie vibaya, akubaliane na kile kitu unachomueleza bila hata ya kuweka kipingamizi. Ukitumia lugha ya ukali, yenye kuonesha dharau na kuona anachokifanya ni cha kijinga, basi jua unakaribisha ugomvi. Utamfanya akuone unamdharau na mtu akishaona anadharaulika, hata kama kitu unachomueleza ni kizuri, anaweza kukipinga tu.

Inahitaji busara, hekima ya hali ya juu ili uweze kumkosoa mwenzi wako. Yawezekana kwa mazingira aliyolelewa, anachokifanya huamini ni sahihi lakini sasa amekuja kwako, mnaanzisha ulimwengu wenu, hivyo inahitajika akili ya ziada kuweza kumbadilisha. Tengeni muda mzuri wa kuelezana mambo mbalimbali ya kudumisha uhusiano wenu. Mzungumze na kusikilizana. Kila mmoja amueleze mwenzake kile anachoamini kinaweza kusaidia kustawi wa penzi lao, kwa kutumia lugha nzuri isiyokuwa na kebehi.

Mnapokuwa kwenye uhusiao, kwanza kila mmoja ajifunze namna ya kujipenda mwenyewe. Unapojua kujipenda mwenyewe na ukajua unahitaji nini ili kuipata furaha yako, basi ni rahisi sana kumtafutia mwenzako pia furaha unayoipata wewe. Usiwe na ubinafsi, furaha unayoipata wewe mpe na mwenzako. Unavyojijali, basi mjali na mwenzako. Kujipenda unavyojipenda basi kwa kiasi hichohicho mpende na mwenzi wako. Ukifanya hivyo, mwenzi wako naye hatakuwa na namna ya kufanya zaidi ya kukurejeshea upendo.Related image

Jifunze kuwa na imani na mwenzako. Unapomjengea mwenzako imani, inamfanya wakati mwingine ashindwe kufanya maovu. Unapomuamini, unamfanya mwenzako ajiheshimu, maana anajua unamuamini na akifanya lolote la kijinga, lazima nafsi yake itamsuta. Muamini mwenzi wako. Mtengenezee mazingira ya kumuamini ili na yeye pia akuamini. Msiishi kwa kufuatiliana, maana maisha hayapo hivyo. Binadamu hawezi kuchungwa kama kondoo au mbuzi. Kubwa linalohitajika ni kujua thamani ya kuaminiana.

Anayekuamini anakujali, anayekujali atakulindia heshima. Hivyo, mkigundua hilo na mkaelekezana kiutu uzima, hakika mtaaminiana. Kila moja awe mkweli na mwaminifu. Ni ukweli pekee utakaowafanya muwe na furaha muda wote. Mkiwa waongowaongo, hamtadumu. Uongo una madhara. Ujanja ujanja ni tatizo katika uhusiano. Kuwa mwaminifu kwa mwenzako, naye pia awe mkweli na mwaminifu.

Kuweni nyinyi, tengenezeni maisha yenu. Msijilinganishe na mtu mwingine. Wekeni mikakati yenu na namna mnavyotaka kuishi, ishini maisha yenu. Mkiyafanya hayo yote, hakika penzi lenu litastawi na mtafurahia maisha ya uhusiano, uchumba na hata ndoa!
Share:

Sababu za wanaume wengi kukimbiwa na wanawake




Imezoeleka katika jamii kwamba wanaume hukimbiwa na wanawake kwa kukosa kipato au alichonacho ni kidogo, au muonekano na maumbile ya mwanaume bila kuzingatia kwamba wanawake huangalia vitu vingine zaidi ili kugundua kama wanaweza kuishi na aina hiyo ya mwanaume.

Zifuatazo ni sababu zinazowafanya wanawake wakimbie mahusiano na wanaume wenye tabia hizi:-

Kulazimishwa au kusukumwa kwenye maamuzi.
Wanawake hupenda mwanaume mwenye msimamo wake na mwenye kufanya maamuzi na kusaidia wenzie wanapohitahi msaada kutoka kwake pamoja nayeye mwenyewe bila shinikizo kutoka kwa yeyote. Usisukumwe sukumwe hovyo hata kama ikiwa na mama yako hili huonyesha udhaifu.

Ulevi wa kupindukia.
Sawa, Unywaji wa pombe haujawahi kupingwa ila endapo mwanaume ni mnywaji kupindukia kiasi anaweza akalala hata baa, akaazisha ugomvi au kuzima kabisa haipendezi. Hakuna kitu wanawake wanachukia kama mwanaume asiwejiweza anapokunywa pombe.

Matusi na lugha chafu.
Inawezekana wote kuna wakati huwa tunajikuta tunatumia maneno makali kama matusi na lugha chafu lakini lakini sasa inapofikia 60% ya maneno yanayotoka mdomoni mwako ni machafu, tena bila hata kuzingatia mahali ulipo, haipendezi tena si kwa mwanamke tu. Wanawake huwafurahia wanaume wanaojua nini aseme na akiseme wapi. Lugha chafu na matusi hayatakufikisha popote kwenye sekta hii ya mapenzi.

Kulalamika kuhusu mpenzi wako wa zamani.
Hamna anayejali kwamba mpenzi wako alikua mdanganyifu, alikuchuna au Malaya, kumlalamikia mwanamke wako wa sasa kuhusu mwanamke mwingine kunazidi kukupunguzia nafasi yaw ewe kuwa na mwanamke wa sasa kwa muda mrefu 1) atafikiri licha ya yote, bado unampenda 2) atafikiri hicho ndicho utakifanya kwa anayefuata baada yake kwa maana kwa sasa unalalamika bila upande wa pili kuwepo hivyo waweza kuwa unadanganya na ndicho utafanya na baada ya mahusiano haya.

Mwanaume king’anganizi mwenye kuhitaji zaidi na zaidi.
Mwanaume analazimisha kupigiwa simu kila baada ya lisaa katika siku? Utadhani isipokua hivyo atafariki, na ukumbuke hapo hata hajawa Boyfriend bado, ndio kwanza anaongea na msichana. Jaribu kutafuta cha kufanya uwe busy kidogo hamna kitu kinakera kama mwanaume ambaye wanawake watafikiri hana kingine cha kufanya zaidi ya kufikiria mwanamke au mapenzi, mpe muda wa kukumiss ili akuze hisia zake kwako inavyotakiwa.

Mtu asiyejali familia wala rafiki zake.
Haitajalisha kabisa hata kama utamfanya yeye ajisikie kama Malkia, kama hujali familia yako hatavutiwa na wewe kwa imani kwamba utamfanyia hivyo nayeye pindi atakapokua mmoja kati ya wanafamilia kama mtafikia hatua ya kuoana. Jitahidi sana uwe na mahusiano mazuri na watu wanaokuzunguka, wanawake huliangalia hilo kwa wakati.

Uongo.
Kusema kweli, uongo kwa wanaume umekithiri, wengi wao huongea na uongo ili wapate wanachotaka vile inaaminika kwao bila longo longo maisha ya siku hizi huwezi kumpata mwanamke, la hasha, endapo mwanamke anagundua umemdanganya kitu, hata kama kilikua kidogo namna gani, imani na wewe inapotea. Hamna uongo mdogo na mkubwa, uongo ni uongo. Na hakuja jinsi ya kujielezea kwanini mtu ulidanganya wakati fulani na sasa unaamua kusema ukweli. Kuwa mkweli wakati wote.
Share:

Njia zitakazowasiaidia muweze kudumu katika mahusiano yenu ya kimapenzi



Hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa pia. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

Zifuatazo ni baadhi tu ya njia mbalimbali za kufanya ukae na mpenzi wako kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mkafurahia mapenzi yenu popote pale mtakapokuwa na mtakapoishi.

1. Kuwa na muonekano chanya kwa mpenzi wako.
Ukiwa ni mtu wa kuangalia mabaya/kasoro sana kwa mpenzi wako kuliko mazuri yake hautakuja kukaa kwenye mahusiano kwa muda mrefu hata siku moja, utaendelea kubadilisha wanaume/Wanawake kila siku na mwisho wa siku utajiona huna bahati kwenye mapenzi na wakati Unayeyaharibu mapenzi yako ni wewe Mwenyewe…kakuna asiye na kasoro (ukiwemo wewe mwenyewe).

Kwa hiyo muonyeshe mpenzi wako mapenzi bora na umrekebishe pale anapokosea Bila kuwa na lawama mara kwa mara, kuna makosa mengine ni hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa in return. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

2. Mpe nafasi na uhuru mpenzi wako.
Mnapokuwa kwenye mahusiano jitahidini kwa hali na mali kupeana nafasi/uhuru kwenye mambo mengi hasa yale ya kitaaluma zaidi na kimaisha. Anapokwambia yupo kwenye kikao cha kikazi jaribu kumuelewa na umpe support ya kutosha kwenye kazi zake au biashara zake au hata masomo yake. Usipende sana kulalamika pale anapochelewa kurudi kazini au kutoka kwenye biashara zake bali mpokee kwa upole na baada ya kupumzika ndipo muulize kwa upole na kimahaba zaidi kwanini siku hizi anachelewa sana kurudi au kwenye biashara zake au shuleni tofauti na zamani.

Hii itajenga zaidi kuliko kubomoa kwa kulalamika na kupayuka mbele yake na huku yeye akiwa hata hajapumzika na itamfanya siku nyingine aione nyumba chungu kitu ambacho si kizuri kwenu wote wawili.

3. Mfanye mwenza wako ajivunie kuwa nawe kila wakati.
Hakikisha katika mapenzi yenu kila siku unamfanya mpenzi wako ajivunie kuwa nawe na hakikisha humfanyi ajute kwa kukuchagua wewe miongoni mwa wote aliowaona. Usijidanganye hata siku moja kuwa kwa kumpata tu na kwa yeye kukupenda basi hajaona mwingine wa kuweza kuwa naye.

Wapo wengi sana anaoweza kuwa nao lakini amekuchagua wewe katika hao wote, kwa hiyo usimfanye aanze kuwafikiria wale wengine wanaomfuatilia kila siku na kumsumbua. Ukianza kumwacha aanze kuwafikiria wengine aidha kwa wewe kuwa unamkosesha amani ya mapenzi kila mara au kwa mengine mabaya ndani ya mapenzi basi ipo siku utaishia pabaya.

4. Msadie kwa hali na mali kila inapowezekana.
Kwenye mahusiano huwa kuna kupanda na kushuka miongoni mwa wapenzi na hasa kiuchumi na hata kisaikolojia. Hakuna kitu kizuri kwenye mapenzi kama mtu kupata tatizo na akasaidiwa na mpenzi wake katika hali ambayo hakuitegemea, namaanisha mpenzi wako akipata tatizo lolote hakikisha wewe ndo unakuwa wa kwanza kulifahamu na kulifanyia kazi.

Sio matatizo yote yanamalizwa kwa pesa so hata ushauri na kumpa mawazo chanya inasaidia sana na kumfanya awe na furaha kuwa nawe. Kama unampenda usione tabu kumsaidia kwa kuogopa kuonekana eti unahonga, huyo ni mpenzi wako kwa hiyo jiamini na umpe kile anachostahili kusaidiwa na mpenzi wake.

Yapo mambo mengi sana ambayo kama mkiyafanya kwenye mapenzi basi uhusiano wenu utakuwa wa kudumu na wenye furaha sana ingawa hapa nimezungumzia kwa uchache sana lakini nina imani itasaidia sana kwa wote walio kwenye mahusiano .

Mapenzi hayana ndumba au limbwata hata siku moja, unapoona wapenzi wengi wana furaha kwenye mapenzi yao ni kwa sababu wanavumiliana kwa mengi na kusameheana kwa mengi. sana na unaweza kuyarekebisha kwa kukaa chini na mpenzi wako mkayamaliza kwa dakika 5 tu lakini wengine huwa issue kubwa kwao na kusababisha mwisho mbaya.
Share:

Mambo muhimu ya kuzingatia kabla ya kujiingiza katika mahusiano ya kimapenzi




Ukweli ni kwamba inachukua muda mrefu kumfahamu mtu vizuri, kikubwa zaidi watu wanabadilika jinsi wanavyokuwa, hela zinaongezeka au kupungua na wanajikuta wanavutiwa na watu wa aina tofauti. Kwa wale ambao hawajabahatika kupata wenza wao kuna mambo ya msingi ya kuzingatia kabla hujajizamisha katika dimbwi la mapenzi, ukizingatia mambo haya, hata kama mtu uliyenaye atabadilika , uwezekano wa kuvumiliana na kuweza kuishi pamoja ni mkubwa zaidi.

1. Ni lengo (ambition),
kama mmoja kati wa wapenzi (nazungumzia wapenzi ambao wanampango wa kuishi pamoja kama mke na mume) ni mtu wa kuwa na malengo na anataka kufanya kitu fulani au kuwa mtu fulani katika maisha yake na mwenzake anachukulia siku kama inavyokuja (laid back), huyu ambaye ana malengo atamchukulia ambaye ni “laid back” kama ni mvivu. Wapenzi wanatakiwa wasipishane sana katika malengo yao hata kama wana kazi mbali mbali.

2. Ni uwazi (openness),
kama mpenzi wako ni “open minded” anapenda kujifunza vitu tofauti, kujaribu vyakula tofauti, kusafiri n.k. Yule ambaye anapenda kujifunza mambo mapya kila siku atamuona mwenzake anaboa.

3. Wapenzi wanaweza kuwa tofauti katika ujuzi wa hisia (emotional intelligence).
Hapa kama tofauti sio kubwa, watu wanaweza kuvumiliana na kuishi pamoja, ila kama tofauti ni kubwa sana, yule ambaye hana ujuzi wa hisia, atakuwa anamburuza na kumharibia mudi yule ambaye amesimama imara kwenye mambo ya hisia. Onyo kwa wanaume ambao wana ujuzi au utaalam wa kusoma hisia za wanawake, wanawake ambao wana F katika ujuzi wa hisia huwa wanavutiwa sana na watu kama ninyi.

4. Ni usosho,
kama mmoja wenu ni mtu wa watu anapenda kuongea na watu na anamarafiki kibao, utamkwaza ambae ni mtu ambaye anapenda maisha “private” na ya utulivu. Mwenzako atakuwa bize anaweka picha zenu na status zinazowahusu facebook wakati wewe unataka mambo ya ndani yawe ya ndani tu. Kama tofauti si kubwa sana mnaweza vumiliana kama tofauti ni kubwa, muda si mrefu mtashindwana

5. Ni wivu.
Wivu ni kitu kibaya sana, kama mpenzi mmoja ana wivu ni ngumu kuekewana na ambaye hana wivu. Kama wote mna wivu, sawa kwani kila mmoja ataepuka kufanya mambo ambayo yanamuumiza mwenzake, ila kama mmoja ndio ana wivu ataona mwenzake hajali, basi ukimuona mwenzako anaongea na classmate wake wa zamani au ukiona mtu amepiga picha na mpenzi wako ameshikwa bega basi inakuwa fujo tupu. Kama upo tayari kwenye uhusiano, na mwenzako ana wivu, jaribu kumuelewesha kwamba kum-kumbatia rafiki yako sio kwamba ndio una mipango mingine ya siri.

Kikubwa katika yote ni uaminifu, kama hamna uaminifu katika mapenzi au ndoa. Usipasue kichwa, ondoka na tafuta mtu ambaye anakuamini au kama haupo tayari kuwa mwaminifu usijiingize katika mahusiano, utajiumiza mwenyewe na mwenzako. Msome mwenzako kabla ya kuanza kuitana wachumba, kama tangu siku ya kwanza mwenzako ana wasiwasi na wewe ukikaribia simu yake, ni afadhali umuulize mapema, kulikoni? Kama umepoteza uaminifu katika mahusiano yako, usihofu, muonyeshe mweza wako kwamba umebadilika na jinsi muda unavyoenda atajifunza kukuamini tena.

Hizi sifa zilizotajwa hapo juu sio za kina sana, lakini ni moja wapo ya mambo ya kuzingatia katika kuchagua mwenza wako wa maisha(kama basi mapenzi yana macho) kabla ya kujizamisha katika mapenzi. Je wewe unaona ni mambo gani ya kuzingatia katika mahusiano na ni mambo gani yanasababisha ndoa kuvunjika? Usisite kuandika maoni yako
Share:

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger