juu

Wednesday 12 June 2019

Jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli

Kuwa msichana
Weka kazi yako binafsi na elimu yako kando. Wanawake wengi wanapokuwa kwenye miadi hupenda kutumia elimu na madaraka yao kulumbana na wenzi wao kupita kiasi. Hupaswi kufanya hivyo, badala yake unatakiwa kujua kwamba hapo mpo kwenye pambano la ngumi au malumbano ya hoja.

Angalia juu ya uzuri wakeUsipumbazike na utanashati wake. Jiulize, mwanaume huyu anastahili kuuteka moyo wako? Ni mzuri kiasi gani katika uhusiano? Anamhudumiaje mama yake? Anaishi vipi na ndugu na rafiki zake? Kama jibu la maswali haya haliko wazi, basi chunguza zaidi.

Mara atakapokuwa na uhakika kuwa wako, anaweza kubadilika na kuendelea na tabia zake za zamani na kukutenda kama anavyowatenda watu wengine.

Jizuie kabla ya kufanya mapenziNashauri kwamba usifanye mapenzi na mwanaume/mwanamke huyo mpya haraka, angalau baada ya kufahamiana naye kwa miezi mitatu hivi, kama lengo ni kuwa naye kwa muda mrefu. Ni vizuri ukakubali kufanya naye mapenzi angalau baada ya kumfahamu vilivyo na yeye mwenyewe akakutamkia jinsi anavyokupenda, vinginevyo anaweza akakuchezea tu!

Nenda na mtiririko
Ufunguo sahihi wa kudumu katika uhusiano wenu kama wapenzi ni kuwa nyote wawili kufikia maafikiano. Kama mpenzi mmoja au nyote wawili mtakuwa mnafanya mambo bila ushirikiano au kutishwa na mabadiliko madogo, matatizo yataanza kuchipua.

Kwa mfano, kama ataanza kufanya kazi na kuchelewa kurudi usiku wakati wewe ukitegemea kumwandalia chakula cha usiku, elewa kwamba atafarijika zaidi kama utamwandalia kahawa kabla ya mlo kamili. Atajilaumu kwa mabadiliko ya mipango na atataka akutamkie yaliyo moyoni mwake ili akuweke kwenye himaya yake.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger