juu

Tuesday 26 November 2019

Kwa njia hizi lazima apagawe




Umekuwa na wakati mgumu hivi karibuni kufurahia ngoma kila siku? Mambo haya yatasaidia kuwasha tena moto wa mapenzi na kukuwezesha kufika kileleni mara kwa mara!

1: Usilenge kileleni, kuna mlima wa kukwea Bidii nyingi kitandani si kiungo pekee cha kumtosheleza mwanamke; kila unapotia bidii ndivyo matokeo yanadidimia. Badala yake, tumia ujuzi zaidi; zingatia shughuli si shabaha. Kushiriki mapenzi si mashindano; achana na hesabu na ujivinjari!

2: Mwili wako kipimo tosha Mwili wako ni kipimo tosha kukuambia iwapo mambo ni shwari au la – acha kufuata kile ambacho mawazo na moyo unakuambia. Weka kando wasiwasi na uzime mijadala akilini mwako. Jifunze kubaini hisia na ashiki za mwili wako, na uzipatie usukani kama inavyotakiwa. Ni baada tu ya kujua kinachozuzua mwili wako ndipo utamwelekeza mwenzio maeneo atakayobonyeza. Habari Nyingine: Maneno sita ya kumfurahisha mpenzi wako

3: Weka kila kitu wazi Baada ya kubaini kinachozuzua mwili wako, jadili na mpenzi wako. Mwanzoni, mjadala huu hautakuwa rahisi lakini ndiyo njia ya pekee kwa yeye kupata ramani ya mwili wako. Usihofu, muambie kila kiungo kinachokuzuzua na atakushuru sana.

4: Imarisha ngoma Mambo mapya huleta uchangamfu na msisimko wa kipekee chumbani. Tupa nje mitindo ya zamani kumbatia mapya! Soma majarida kisha ujadiliane na mpenzi wako mitindo mipya utakayodondoa hapo, asije akadhania umetumbukia katika ponografia ama kuna jamaa anamfunza moja kwa moja. Habari Nyingine: Sababu nne kuu za wanandoa kulala pamoja

5: Kuwa na imani Kila kitu hutendeka kwa imani, hata kushiriki mapenzi. Uko na haki zote za kujivinjari; Mungu mwenyewe aliumba ngono kwa sababu anataka ufurahie mahaba!
Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger