juu

Tuesday 19 November 2019

Njoo Ufahamu Mavazi Unayotakiwa Kuyavaa Ukiwa Chumbani na Mwenza Wako Ambayo Yatasaidia Kupandisha Hisia



Najua leo ni siku ya mapumziko kwa watu wengi na ni siku ambayo familia inatulia nyumbani na ndo wakati mzuri kwa wapenzi kuwa karibu na kujiachia leo tuongee kuhusu mavazi gani ya kuvaa ukiwa na mwenzi wako chumbani.

Mapenzi ni hisia,na hisia hizo huwa kwa wote yaani kwa wanaume pamoja na wanawake,baadhi ya walio kwenye uhusiano huwalalamikia sana wenzi wao na sababu kuu huwa ni kutokuwa na hamu ya kufanya nao tendo la ndoa.Hapa nitazungumzia mavazi yanayopaswa kuvaliwa chumbani hasa mnapokuwa wawili tu yaani mke na mume..

Mwanaume siku zote huwa na hisia za haraka sana hasa ukimjulia,lakini baadhi ya wanawake huwa wanashindwa kuzijua haraka mbinu za kumpandisha mzuka mumewe hata kama amechoka au ana hasira kwa siku hiyo…

Ndugu yangu uchawi rahisi kwa mumeo ni kumvalia nguo nyepesi na yenye kuonyesha maumbile yako kamili,hii inaweza kuwa gauni nyepesi inayoonyesha maumbile yako ama siku hizi kuna mitandio milaini ambayo pia unaweza kuivaa pindi unapokuwa na mwenzi wako,ikumbukwe pia wanaume wengi hupatwa na tatizo la ukosefu wa nguvu za kiume kwa kukosa hisia za kufanya tendo hilo lakini wanawake ni dawa nzuri ya tatizo hilo ikiwa ataweza kumuhamasisha mumewe kwa njia mbalimbali ikiwemo ya vazi ambalo litamfanya mzee asisimke..

Ntakushangaa utaposhangaa mumeo hana hamu na wewe kwakuwa muda wote wamvalia madera ukikaa utafute anayekuroga utajipotezea muda mchawi ni wewe mwenyewe ambaye unashindwa kujiongeza ata mnapokuwa chumbani wawili.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Translate

sam magelle

Main Menu Links

HABARI KALI ZAIDI

HABARI ZILIZOPITA

CHAGUA HABARI na sammagelle.com

Copyright © juu | Powered by Blogger